#Local News

BUNGE LAFUTILIA MBALI VIKAO VYA LEO

Bunge limefutilia mbali vikao vyake vya leo ili kuwawezesha wabunge kuhudhuria ibada ya wafu kutoa heshima zao za mwisho kwa aliyekuwa mwenzao wa Emurua Dikirr Johana Ng’eno, aliyefariki Jumamosi na watu wengine watano kwenye ajali ya ndege.

Kiongozi wa walio wengi bungeni Kimani Ichung’wa, aliweka wazi tangazo hilo wakati wa vikao vya jana, akisema hatua hiyo itawapa wabunge fursa ya kumwomboleza mwenzao.

Mbunge huyo atazikwa Ijumaa katika eneo bunge lake.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *