#Local News

IEBC YAONYA KUHUSU UTAPELI WA AJIRA

Tume huru ya uchaguzi na mipaka, IEBC, imetoa tahadhari kwa umma kuhusiana matangazo ya ulaghai yanayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu nafasi za ajira katika tume  hiyo.

Kupitia tangazo, IEBC imefafanua kwamba matangazo hayo ni ya udanganyifu, na kusisitiza kwamba nafasi za ajira katika tume hiyo hutolewa tu kupitia tovuti yake rasmi.

Imewataka wakenya kuwa macho dhidi ya matapeli.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *