SAKAJA: MFUMO WA MAJITAKA FINYU
Gavana wa kaunti ya Nairobi Johnson Sakaja amekariri kuwa mfumo wa majitaka katika jiji la Nairobi hauwezi kuhimili kiwango cha mafuriko, hatua anayosema itatatuliwa kupitia kwa mkataba wa ushirikiano kati ya serikali yake na ile ya kitaifa.
Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga, Sakaja amesisitiza kuwa mfumo wa mapato ya kaunti pekee hauwezi kutoa suluhisho kwa changamoto hizo za mara kwa mara jinsi ilivyo kwa kaunti nyingine.
Ametoa hakikisho kwamba ushirikiano wa hivi majuzi utatoa suluhu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































