USIKU MKUBWA ULAYA, MECHI ZA AWAMU YA 16
Ni usiku mwingine wa kinyang’anyiro cha klabu bingwa bara Ulaya ambapo jumla ya mechi 4 za raundi ya 16 zitachezwa leo usiku, huku nyingine 4 zikisakatwa hapo kesho, ukiwa ni mkondo wa kwanza.
Liverpool watarejea kikaangoni nchini Uturiki kumenyana na Galatasaray, walikocharazwa bao 1-0 katika awamu ya makundi msimu huu.
Mechi nyingine itajumuisha Newcastle, ambao wataialika Barcelona huku Atletico Madrid wakiwa wenyeji wa Tottenham.
Atalanta, mwakilishi wa pekee wa Italia katika kipute hicho, watasakata dhidi ya miamba wa Ujerumani, Bayern Munich.
Mkondo wa mwisho utachezwa wiki ijayo ili kusaka tiketi ya kuingia robo fainali.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































