BAJETI YA ZIADA YA IEBC YAIBUA MASWALI
Wabunge wameibua maswali kuhusu mahitaji ya shilingi milioni 888 za ziada ya tume huru ya uchaguzi na mipaka, IEBC, ambazo tume hiyo inasema zitatumika kwa maandalizi ya uchaguzi mkuu ujao.
Kwa mujibu wa IEBC, fedha hizo zitatumika kuwasajili wapiga kura wapya, kujenga kituo cha mawasiliano, ununuzi wa magari mapya ya makamishna na kumlipa afisa mkuu mtendaji aliyeondoka Marijan Hussein Marijan.
Hata hivyo, wabunge wametilia shaka mahitaji hayo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































