#Local News

VIJANA WATARAJIA AJIRA ZA SGR

Mamia ya vijana nchini wanatarajiwa kunufaika na nafasi za ajira kwenye mradi wa ujenzi wa awamu ya pili ya reli ya kisasa, SGR, kutoka Naivasha kuelekea Malaba kupitia Kisumu ambao umeratibiwa kukamilishwa ndani ya miaka 2.

Akizungumza baada ya kuzindua mradi huo wa shilingi bilioni 500, Rais William Ruto amesema kuwa reli hiyo itarahisisha usafirishaji wa mizigo na abiria kuelekea Magharibi mwa nchi.

Reli hiyo itajengwa awamu 2 za 2B na 2C, 2C ikitoka Narok hadi Kisumu huku 2B ikipita Kisumu, Siaya, Vihiga, Kakamega hadi Busia.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *