WALIOANGAMIA KWENYE AJALI KISII KUZIKWA LEO
Watu 6 waliouawa kupitia ajali ya barabara katika eno la Kegati kwenye barabara ya Kisii-Keroka wiki mbili zilizopita watazikwa hii leo katika hafla tofauti kwenye eneo bunge la Nyaribari Chache.
6 hao waliangamia baada ya trela lililoripotiwa kukata breki, kupoteza mwelekeo na kuwagonga katika soko la Kegati.
Ibada ya pamoja ya mazishi kwa 6 hao itaandaliwa katika shule ya msingi ya Kegati.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































