EACC YAONYA WANASIASA DHIDI YA MATUMIZI MABAYA YA MALI YA UMMA
Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi nchini (EACC) imetoa onyo kwa wanasiasa walio madarakani dhidi ya kutumia mali ya umma kuendesha kampeni zao.
Wakizungumza jijini Nakuru , viongozi wa tume hiyo wamesisitiza umuhimu wa uadilifu katika utumizi wa rasilimali za umma.
Aidha, wameeleza kuwa ufisadi umeorodheshwa kama janga la pili nchini baada ya tatizo la ukosefu wa ajira.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































