HARVEY BARNES KUCHUKUA NAFASI YA EZE KATIKA TIMU YA UINGEREZA
Mchezaji wa Newcastle, Harvey Barnes, anatarajiwa kuitwa katika kikosi cha England chini ya Thomas Tuchel kuchukua nafasi ya Eberechi Eze aliyejeruhiwa.
Eze hakuwemo katika kikosi cha Arsenal katika fainali ya Carabao Cup Jumapili ambapo walipoteza 2-0 dhidi ya Manchester City kutokana na jeraha la mguu wa chini.
Barnes tayari amewahi kuitwa mara moja mnamoOktoba 2020, ikiwa ni mchezo wa kwanza na wa pekee katika kikosi cha England kwenye mechi ya kirafiki dhidi ya Wales.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































