MAGEUZI YA POLISI YAFIKIA ASILIMIA 55
Katibu Mkuu wa Usalama wa Ndani, Raymond Omollo, amesema Kenya imefikia utekelezaji wa asilimia 55 ya mageuzi ya polisi yanayoendelea nchini kufuatia mkutano wa ngazi ya juu wa kamati ya usalama wa taifa.
Mageuzi hayo, yaliyoanzishwa kwa maelekezo ya rais, yanalenga kuimarisha taasisi za usalama, kuboresha utoaji huduma na kuboresha mifumo ya kipolisi kote nchini.
Omollo amesema maendeleo makubwa yamepatikana katika maeneo muhimu ikiwemo utawala, sheria na ustawi wa maafisa wa polisi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































