#Local News

KENYA YAJIUNGA NA MPANGO WA KIMATAIFA WA AFYA

Katika juhudi za kupunguza vifo vya watoto wachanga, Kenya imetangaza kujiunga na mpango wa kimataifa wa afya kwa muda wa miaka 5, mpango utakaogharimu kima cha shilingi bilioni 11.

Kulingana na mkurugenzi mkuu wa idara ya afya Daktari Patrick Amoth, mpango huo utatekelezwa katika kaunti 12 ambazo huchangia asilimia 50 ya vifo hivyo, akisema kaunti ya Nakuru itakuwa ya kwanza kunufaika.

Miongoni mwa kaunti nyingine ni Trans Nzoia, Kakamega, Kisumu, Nairobi, Mombasa na Uasin Gishu.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *