#Football #Sports

RISING STARLETS MBIONI KUFUZU FIFA U17

Timu ya taifa ya chipukizi ya wanawake, Rising Starlets, imeingia kambini kwa matayarisho ya mechi za kufuzu mashindano ya kombe la dunia kwa wachezaji wa umri usiozidi miaka 17, yaani FIFA World Cup U17.

Kenya itachuana na Namibia tarehe 12 mwezi ujao kwa mkondo wa kwanza nchini Namibia, kabla ya marudiano wiki moja baadaye jijini Nairobi.

Kocha mkuu wa Rising Starlets Mildred Cheche, amesema kikosi chake kimewajumuisha wachezaji wenye uzoefu, na wale wanaoinukia, akiongeza kuwa ana imani kuwa wachezaji hao wataisaidia Kenya kuafikia ndoto ya kufuzu kombe la dunia.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *