#Local News

UPINZANI: RUTO ANATAKA KUWATUMIA WAFU KUSHINDA

Viongozi wa muungano wa upinzani wameratibiwa kuendelea na ziara yao katika eneo la Ukambani hii leo, baada ya kuanza ziara hiyo hapo jana katika kaunti ya Makueni.

Kwenye ziara hiyo, viongozi hao wameibua madai kwamba Rais William Ruto ana nia ya kujilazimishia ushindi kwenye uchaguzi mkuu ujao kwa kutumia kura za wakenya waliofariki ila maelezo yao yangali kwenye sajili ya tume huru ya uchaguzi na mipaka, IEBC.

Wameshinikiza sajili ya wapiga kura kusafishwa ipasavyo.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *