KINDIKI AWATAKA MABALOZI KUITANGAZA KENYA
Naibu Rais, Kithure Kindiki, amewataka mabalozi wa Kenya kuitangaza nchi kama salama na yenye fursa za uwekezaji, akisema ni jukumu lao kuvutia wawekezaji na wageni.
Akizungumza wakati wa kufunga kongamano la 19 la mabalozi jijini Nairobi, Kindiki amesisitiza umuhimu wa mabalozi kushiriki kikamilifu katika kukuza taswira ya taifa kimataifa.
Aidha ameongeza kuwa Kenya imepiga hatua kubwa kiuchumi, na kuhimiza juhudi zaidi za kutangaza mafanikio hayo ili kuchochea uwekezaji na maendeleo ya nchi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































