#Local News

WETANG’ULA ATISHIWA KESI MAHAKAMANI

Kundi la Linda Mwananchi limetishia kumshtaki Spika wa Bunge la Kitaifa, Moses Wetang’ula, kwa kumfurusha Mbunge wa Kitutu Chache Kusini, Anthony Kibagendi, kutoka vikao vya bunge.

Viongozi hao wamedai kuwa hatua hiyo ilikiuka uamuzi wa mahakama uliotaka mbunge huyo arejeshwe bungeni baada ya kuondolewa awali.

Kibagendi alitimuliwa kutokana na matamshi yake kuhusu ufisadi bungeni, suala ambalo sasa limeibua mvutano mpya wa kisheria na kisiasa.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *