MOTO WATEKETEZA NYUMBA ZA MAGEREZA LANG’ATA
Idara ya magereza nchini imethibitisha kuwa moto umeteketeza nyumba 30 za makazi ya maafisa katika Gereza la Wanawake la Lang’ata lenye ulinzi mkali.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na idara hiyo moto huo ulizuka Jumatano jioni majira ya saa moja na nusu na kuteketeza nyumba hizo kabisa.
Hata hivyo, idara hiyo imesema hakuna mtu aliyepoteza maisha au kujeruhiwa, huku kikosi cha dharura kikifanikiwa kudhibiti moto huo na kuzuia usienee zaidi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































