VITUO 30 VYA AFYA KUSHTAKIWA KWA ULAGHAI WA SHA
Wamiliki na wakurugenzi wa vituo 30 vya afya wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za ulaghai iwapo Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma atatoa idhini ya mashtaka hayo.
Kurugenzi ya Upelelezi wa Jinai imesema uchunguzi wa malalamishi ya ulaghai pamoja na ukaguzi wa kitaalamu wa miamala ya vituo hivyo umebaini kuwa wote wana kesi ya kujibu.
Tayari vituo 18 vya afya pamoja na watu 50 wamefikishwa mahakamani wakikabiliwa na mashtaka ya ulaghai.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































