HALI YA MAANDAMANO NCHINI
Hali ya taharuki imetanda katika mengi ya maeneo nchini huku biashara nyingi zikifungwa kufuatia maamndamano ya vijana wa kizazi cha Gen Z.
Jiji Nairobi, waandamanaji wamefunga barabara ya Moi Avenue karibu na eneo la Kencom katikati mwa jiji kwa kutumia mawe, polisi wakilazimika kuwatawanya kwa vitoza machozi.
Jijini Nakuru, waandamanaji wanaendeleza mchezo wa paka na panya na maafisa wa polisi, hali sawa ikishuhudiwa jijini Mombasa na Kisumu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































