MGOMO: WAGONJWA MTRH WAHANGAIKA
Shughuli za matibabu katika hospitali ya rufaa na mafunzo ya Moi jijini Eldoret zimesambaratika kutokana na mgomo wa madaktari ambao umeanza hii leo, madaktari wakiapa kutorejea kazini hadi malalamishi yao yatakapoangaziwa.
Miongoni mwa malalamishi ya madaktari hao ni wenzao kukaa kwa mkataba kwa muda mrefu bila kupewa ajira ya kudumu.
Haya yanajiri huku wagonjwa wakihangaika kutokana na kukwama kwa shughuli zote za matibabu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































