#Local News

ODM MBIONI KUOKOA CHOMBO

Chama cha ODM kimeratibiwa kuendelea na mkutano wake wa kamati ya utendaji hii leo katika kaunti ya Mombasa ambapo chama hicho kinalenga kuimarisha miundo ya kuzuia misukosuko inayotishia kukisambaratisha.

Mkutano huo unalenga kutathmini mikakati ya uhamasishaji katika kujiimarisha mashinani mbali na kujadili masuala yaliyoibuliwa kwenye vikao vya hivi punde vya ushirikishaji wa vijana katika kaunti kadhaa.

Mwenyekiti wa kitaifa Gladys Wanga, amekariri kuwa ODM ingali imara.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *