KANG’ATA ABASHIRI MWANGUKO WA UDA
Gavana wa Murang’a Irungu Kang’ata amesema kuwa chama tawala cha UDA kimepoteza umaarufu katika eneo la Mlima Kenya, na kwamba kitaporomoka kuelekea uchaguzi mkuu ujao.
Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga, Kang’ata amesema mabadiliko ya kisiasa yanayoendelea yamesababisha chama hicho kupoteza umaarufu wake.
Kauli yake inajiri saa chache baada ya awali kutangaza kuwa hatawania muhula wa pili kwa chama cha UDA.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































