BIDCO WATATAFUTA KUVUNJA MSURURU WA MECHI BILA USHINDI

Bidco United wanatafuta kumaliza msururu wa mechi 12 bila ushindi watakapowakaribisha Kakamega Homeboyz alasiri ya leo mjini Murang’a, huku michuano ya Kenya Premier League ikirejea baada ya mapumziko ya FKF Cup. Bidco, walioko nafasi ya 19 wakiwa na pointi 16, wanahitaji ushindi kwa dharura ili kujinasua kutoka eneo la kushuka daraja. Ni tofauti ya pointi […]

SAKAJA AWAHAKIKISHIA WANA NAIROBI RAGA YA KIMATAIFA

Gavana wa Nairobi, Johnson Sakaja, amewaambia wakazi kuwa jiji limejiandaa kikamilifu kupokea duru ya ufunguzi ya mashindano ya HSBC World Rugby SVNS 2 hapo kesho katika uwanja wa Nyayo Mashindano hayo ya siku mbili yanafanya Nairobi kuwa kituo cha raga ya kimataifa, huku timu, maafisa na mashabiki kutoka duniani kote wakijumuika kwenye jijini. Hii ni fursa ya kuonyesha uwezo […]

SERIKALI YAHAKIKISHIA FAMILIA YA SHANTEL HAKI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Jinsia na Uwezeshaji, Anne Wang’ombe, amewahakikishia wakazi kuwa haki itatendeka haraka kufuatia mauaji ya kinyama ya msichana wa miaka tisa, Shantel Waruguru, aliyedaiwa kuuawa na jamaa yake mwishoni mwa wiki iliyopita. Wang’ombe ametoa kauli hiyo alipowatembelea wanafamilia wa marehemu katika kijiji cha Kianjogu, eneobunge la Mathira, ambako huzuni na hasira […]

WAMALWA AWAKARIBISHA SIFUNA NA WENZAKE DAP-K

Kiongozi wa chama cha Democratic Action Party Eugene Wamalwa, amewaalika Katibu Mkuu wa ODM Edwin Sifuna, Mbunge wa Saboti Caleb Amisi na Seneta wa Vihiga Godfrey Osotsi kujiunga na chama cha DAP-K. Wamalwa amesema viongozi hao watapokelewa DAP-K iwapo wataondolewa katika chama cha ODM kwa kusimamia misimamo yao ya kisiasa. Kiongozi huyo wa DAP-K amesema yuko pamoja na […]

RUTO KUELEKEA ETHIOPIA MKUTANO WA AU

Rais William Ruto ataondoka kuelekea Addis Ababa, Ethiopia, kwa Mkutano wa 37 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika. Mada kuu ya mkutano huo ni kujenga mifumo thabiti ya elimu kwa ajili ya rasilimali watu ya karne ya 21 barani Afrika. Rais Ruto atazungumzia kuhusu ukosefu wa usawa wa elimu ambao umewaacha […]

RUKU AMKOSOA OGINGA KWA KUDAI WADHIFA WA NAIBU RAIS

Baadhi ya viongozi kutoka eneo la Mlima Kenya wamekosoa hatua ya kinara wa ODM Oburu Oginga kubadili msimamo na kutangaza kwamba chama hicho kinalenga wadhifa wa naibu Rais kama sehemu ya ushirikiano na chama cha UDA kwenye uchaguzi mkuu ujao, wakisema wadhifa huo utaendelea kushikiliwa na naibu Rais Kithure Kindiki. Waziri wa utumishi wa umma […]

EACC YAANZISHA UCHUNGUZI DHIDI YA UBADHIRIFU VIHIGA

Tume ya maadili na kukabili ufisadi EACC imeanzisha uchunguzi katika madai ya ubadhirifu wa shilingi milioni 5 zilizotumika kwenye hafla ya ufunguzi wa makazi rasmi ya spika wa bunge la kaunti ya Vihiga. Kwenye waraka kwa karani wa bunge hilo, EACC imelitaka bunge hilo kuwasilisha kwa dharura stakabadhi na taarifa ili kufanikisha uchunguzi huo. Miongoni […]

ATLETICO MADRID WANUSIA UBINGWA WA COPA DEL REY

Mabao ya Ademola Lookman, Antoine Griezman na Julian Alvarez yaliwapa Atletico Madrid ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Barcelona katik a mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya dimba la Copa del Rey, na kuwapa harufu ya ubingwa wa taji hilo wanapojiandaa kusaka tiketi ya kuingia fainali watakapovaana kwa mkondo wa pili. Masaibu ya Barca […]

GUNNERS WAFUMWA NA THE BEES, WAYUMBA EPL

Washika bunduki wa Arsenal maarufu kama Gunners walishindwa kuhimili mishale ya nyuki wa Brentford jana usiku, na kupoteza nafasi ya kipekee ya kurejesha uongozi wa alama 6, ligi kuu ya soka nchini Uingereza, EPL ikishika kasi. Bao la Keane Lewis-Potter katika dakika ya 71 ya mchezo lilididimiza matumaini ya Arsenal kubeba taji la EPL msimu […]

KENYA INAUNGA MKONO AFCON 2027 IAHIRISHWE- LOC

Mmojawapo wa wenyeji wa dimba la mataifa bingwa barani Afrika AFCON 2027, Kenya, inaunga mkono kuahirishwa kwa dimba la mwaka ujao hasa kuhusiana na vurugu zinazohusiana na uchaguzi ambazo huenda zikatokea wakati wa mechi hizo. Hii ni kauli ya mwenyekiti wa kamati andalizi ya mechi hizo humu nchini Nicholas Musonye, akiliambia shirika la habari ya […]