GACHAGUA ASEMA RUTO LAZIMA AONDOKE 2027

Aliyekuwa Naibu Rais, Rigathi Gachagua, amepuuzilia mbali mjadala unaoendelea kuhusu nani atakayekuwa mgombea mwenza wa Rais William Ruto katika uchaguzi wa 2027, akisema mjadala huo hauna maana. Gachagua amesema mjadala huo unalenga kupotosha Wakenya, hasa kutoka eneo la Mlima Kenya, na kuondoa umakini wao katika masuala muhimu yanayowahusu. Aidha, ameongeza kuwa iwapo Ruto atamchagua Gladys Wanga […]

MIKAKATI YA RBA YA KULINDA PENISHENI

Mamlaka ya Mafao ya Kustaafu (RBA) imeanzisha mikakati mipya ya kukabiliana na ongezeko la tatizo la michango ya pensheni isiyolipwa, ikiwa ni pamoja na adhabu kali na hatua zinazoweza kuzuia taasisi zinazokiuka sheria kupata fedha za serikali. Chini ya mageuzi hayo, Mamlaka ya Ushuru ya Kenya (KRA) itachukua jukumu kuu katika kufuatilia na kurejesha michango ya […]

DROO YA FA CUP 5TH ROUND

Droo ya raundi ya 5 ya dimba la FA Cup nchini Uingereza ilikamilika hapo jana, huku zawadi ya klabu ya Mansfield ya League One kuibandua Burnley ya ligi kuu, EPL, na kutinga awamu ya 5 ya FA baada ya miaka 50 ikiwa ni kukutanishwa na viongozi wa EPL Arsenal katika uwanja wa One Call. Manchester […]

TIMU 8 KUFAHAMU WAPINZANI KWENYE ROBO FAINALI CAF LEO

Klabu 8 zilizotinga awamu ya robo fainali ya klabu bingwa barani Afrika CAF Champions League zitafahamu wapinzani wao kwenye droo itakayofanyika hii leo jijini Cairo, Misri kufuatia kukamilika kwa awamu ya makundi Jumapili. Timu hizo zilikuwa kwenye makundi 4, ya kwanza na ya pili zikifuzu robo fainali. Miamba wa soka barani wamefuzu awamu hiyo, huku […]

SERIKALI YAANZISHA UJENZI WA THIKA STADIUM

Serikali imeanzisha ujenzi wa uwanja wa Thika Stadium wenye uwezo wa kuwabeba mashabiki 10,000, ambao huenda ukatumiwa kwa mazoezi wakati wa dimba la mataifa bingwa barani Afrika mwaka ujao, AFCON 2027. Ujenzi huo umekadiriwa kugharimu shilingi milioni 850, serikali ikisema utakamilika kufikia mwishoni mwa mwaka huu. Thika Stadium inatarajiwa kuchukua mahala pa Thika Municipal Stadium […]

SAFARI ZA NDEGE ZASAMBARATIKA

Shughuli za usafiri katika viwanja vya ndege nchini zinatarajiwa kuendelea kutatizika kutokana na mgomo wa wafanyakazi wa viwanja hivyo ambao wameapa kuendelea na mgomo wao licha ya agizo la mahakama kuwataka wasitishe mgomo huo. Hapo jana, wasafiri walilazimika kusalia ndani ya ndege huku wengine wakifutilia mbali safari zao kutokana na ukosefu wa wafanyakazi wa kudhibiti […]

FAMILIA, WANAHARAKATI WASHINIKIZA HAKI KITENGELA

Wanaharakati na familia ya Vincent Ayomo, mwanamme aliyeuawa Jumapili iliyopita katika eneo la Kitengela kwenye mkutano ulioongozwa na katibu mkuu wa ODM Edwin Sifuna, wameshinikiza uchunguzi wa kina kufanywa ili wapate haki. Ikiongozwa na mjane wake Winnie Ayomo, familia hiyo imesisitiza kuwa jamaa yao aliuawa na polisi waliiokuwa wakiutawanya umati, huku wanaharakati wakimtaka Waziri wa […]

UPINZANI KUONGOZA MAANDAMANO YA WATU 100,000 NAIROBI

Viongozi wa upinzani nchini wametangaza kuongoza maandamano makubwa jijini Nairobi Ijumaa wiki hii kushinikiza kuwajibishwa kwa maafisa wa polisi wanaoaminika kuvuruga ibada iliyokuwa ikihudhuriwa na aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua mwezi jana kaunti ya Nyeri, baada ya juhudi zao kukutana na Inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja kufeli hapo jana. Wakizungumza kwenye mkutano uliosambaratishwa na […]

MAHAKAMA KUTOA UAMUZI KWENYE KESI YA MVUVI NAKURU

Maafisa 6 wa idara ya wanyamapori nchini KWS wanaohusishwa na kutoweka kwa mvuvi Brian Odhiambo mwanzoni mwa mwaka jana katika mbuga ya wanyama ya Lake Nakuru watafahamu iwapo wana kesi ya kujibu au la tarehe 3 mwezi ujao. Kulingana na hakimu mkuu wa mahakama ya Nakuru Kipkurui Kibelion, mahakama itazingatia ushahidi uliotolewa na upande wa […]

SERIKALI INACHUNGUZA ‘MGENI’ ALIYEWAHADAA WANAWAKE

Hofu imeibuka kuhusiana na usalama wa wanawake nchini kutokana na ripoti ya raia mmoja wa kigeni kudaiwa kuwahadaa wanawake kadhaa na kuwapeleka katika makazi yake nchini, akarekodi na kusambaza picha za siri za wanawake hao bila idhini yao wala ufahamu wa idara ya ujasusi. Kulingana na msemaji wa serikali Isaac Mwaura, idara ya usalama, upelelezi […]