WANAFUNZI WA GRADE 10 KUANZA MASOMO WIKI IJAYO

Wanafunzi wa gredi ya kumi wanatarajiwa kuanza rasmi masomo yao wiki ijayo, kufuatia kusambazwa kwa vitabu vya shule za sekondari ya juu kote nchini. Taasisi ya Mtaala Nchini (KICD) pamoja na Wizara ya Elimu zimesema kuwa wachapishaji tayari wamechapisha vitabu na kusambaza asilimia 50 ya vifaa vya masomo. Hii hatua inahakikisha kuwa wanafunzi wanakuwa tayari […]

ARSENAL KUMENYANA NA MAN UNITED EPL

Ligi Kuu ya Uingereza inaendelea kesho na mechi kadhaa kuchezwa katika viwanja mbalimbali. Mechi ya mapema itashuhudia West Ham wakikabiliana na Sunderland, huku baadaye Man City wakicheza na Wolves, Tottenham wakipambana Burnley kwenye uwanja Turf Moor, Fulham watakuwa wenyeji wa Brighton, huku Liverpool wakiwa wageni wa Bournemouth kwenye Vitality Stadium. Jumapili mechi nyingine zitachezwa ikiwa ni Crystal Palace wapambane na  Chelsea, Newcastle wavaane na Aston Villa kwenye uwanja wa  St. […]

CASEMIRO KUONDOKA MANCHESTER UNITED MWISHONI MWA MSIMU

Klabu ya Manchester United imetangaza kuwa Casemiro ataondoka klabuni mwishoni mwa msimu kufuatia mkataba wake kumalizika. Nahodha huyo wa Timu ya Taifa ya Brazil alijiunga na United kutoka Real Madrid mwaka 2022 na hadi sasa amecheza mechi 146, na kufunga mabao 21 pamoja na kushinda Taji la FA na Carabao. Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

LIGI KUU YA KENYA KUENDELEA KESHO

Ligi Kuu ya Kenya inarejelewa hapo kesho na mechi kadhaa kuchezwa. APS Bomet itakuwa mwenyeji wa Shabana, huku Kariobangi Sharks wakiwa wageni wa Bandari mechi hizo mbili zikisakatwa saa nane Baadae saa kumi Bidco United watakuwa wenyeji wa viongozi wa ligi, Gor Mahia. Jumapili kutakua na michezo kadhaa  pamoja na KCB kucheza nyumbani dhidi ya Tusker, Ulinzi Stars kuwa wenyeji wa Muranga […]

BANDARI FC YAZINDUA TENA NDOTO ZA UBINGWA WA KPL

Msaidizi wa kocha wa Bandari , Razak Siwa, anaamini kuwa The Dockers wameanzisha tena ndoto zao za ubingwa wa Ligi Kuu ya Kenya kufuatia ushindi wa 2-1 ugenini dhidi ya Tusker FC mwishoni mwa wiki iliyopita. Kikosi cha Mombasa kipo nafasi ya kumi kwenye jedwali la KPL, likikusanya alama 23 kutokana na mechi 16, ikiwa pointi 10 nyuma ya […]

BENSON KIPRUTO AONYA MAPEMA KABLA YA BOSTON MARATHON

Mshindi wa zamani wa Boston Marathon, Benson Kipruto, amewaonya wapinzani wake kujiandaa kwa ubishani mkali wakati atakaporudi kwenye mashindano ya Boston mwezi Aprili, akitangaza kuwa yuko tayari kuanza msimu wa 2026 akipambana na mashujaa wengine wa ngazi ya juu wa wanaume. Tukio la Boston Marathon la 130, litafanyika Aprili 20 huku mshindi wa mwaka jana John […]

FAMILIA YATAKA HAKI KUFUATIA KIFO CHA ALPHY MIGASHA

Familia ya Alphy Migasha inataka kukamatwa mara moja na kufikishwa mahakamani kwa afisa wa kijeshi anayeshukiwa kumuua ndugu yao baada ya kumpiga kikatili katika mtaa wa Umoja One, jijini Nairobi. Haya yanajiri huku ripoti ya uchunguzi wa maiti ikibainisha kuwa Alphy alifariki kutokana na gando la damu kwenye mapafu liliLOtokana na majeraha aliyoyapata marehemu wakati wa […]

MARAGA AIBUA WASIWASI KUHUSU UENDELEVU WA MPANGO WA NYOTA

Aliyekuwa Jaji Mkuu na mgombea wa urais, David Maraga, ameikosoa serikali kuhusu mpango unaoendelea wa NYOTA, akisema kuwa utekelezaji wake unatiliwa shaka. Maraga amehoji uendelevu wa mpango huo, pamoja na namna shilingi elfu hamsini zinazotolewa kwa wanufaika, akisema huenda zikadhoofisha kufikiwa kwa lengo kuu la mpango huo na kuupa taswira ya kisiasa badala ya maendeleo […]

JSC YATEUA WAGOMBEA 15 WA MAJAJI WA MAHAKAMA YA RUFAA

Tume ya Huduma za Mahakama, JSC, imeteua jumla ya wagombea kumi na tano kwa ajili ya kuteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama ya Rufaa, kufuatia kukamilika kwa mchakato mkali na wenye ushindani mkubwa wa usaili. Miongoni mwa walioteuliwa ni Mwenyekiti wa Mamlaka Huru ya Usimamizi wa Polisi, IPOA, Issack Hassan, pamoja na wakili mwandamizi Katwa Kigen, […]

NDINDI NYORO ATAKA ELIMU YA SEKONDARI IWE BURE KIKAMILIFU

Mbunge wa Kiharu, Ndindi Nyoro, ametoa wito wa kutekelezwa mara moja kwa elimu ya sekondari bure kikamilifu nchini Kenya, akisema kuwa elimu inapaswa kulindwa dhidi ya ushawishi wa kisiasa. Akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara, Nyoro alipendekeza kuanzishwa kwa hazina ya kitaifa ya elimu ya sekondari itakayofadhili shule za kutwa pamoja na chakula cha wanafunzi […]