MZOZO WA ARDHI TRANSMARA

Wanakijiji   katika mpaka wa Transmara na Migori wanalilia serikali kuwanusuru dhidi ya watu  walio na lengo la kuwafurusha katika makao yao  kwa njia ya mkato. Wenyeji hao   wanadai kuhangaishwa na wanaomezea mate ardhi hiyo huku wakidai zaidi ya vijana 15 wakikamatwa kiholela kufuatia mzozo wa mara kwa mara kuhusu mashamba yaliyoko katika mpaka huo. Sasa wanaomba maafisa wakuu […]

RUKU AWAHAKIKISHIA WAKAZI WA TANA RIVER MSAADA WA SERIKALI

Waziri wa utumishi wa umma  Geoffrey Ruku amewahakikishia wakazi wa kaunti ya Tana river ahadi ya serikali ya kusaidia familia zilizoathiriwa na hali mbaya ya ukame . Akizungumza wakati wa usambazaji wa chakula cha msaada, waziri huyo amesema serikali inafanya kazi kusaidia familia 180 . Ruku amebainisha kuwa utoaji wa chakula cha msaada umehitajika kutokana na ukame unaoendelea, na kuziacha familia nyingi […]

WAHALIFU WAWILI WAKAMATWA KISUMU

Wanaume wawili wamekamatwa Kisumu baada ya polisi kupata silaha na vitu vinavyoaminika kutumika katika shughuli za  uhalifu . Katika taarifa iliyochapishwa kwenye ukurasa wa  x  , polisi wamesema watu hao   walikamatwa kwenye kivuko cha reli huku wakidaiwa kujiandaa kufanya uhalifu katika eneo hilo. Operesheni hiyo ilizinduliwa baada ya wakazi kutoa tahadhari kuhusu mienendo yenye mashaka karibu na barabara yenye shughuli nyingi, […]

MANCHESTER CITY YASHINDWA, REAL MADRID NA ARSENAL WASHINDA

Manchester City walipoteza kwa 3-1 dhidi ya Bodo/Glimt, huku klabu ya Norway ikisababisha mojawapo ya matukio makubwa zaidi ya kushangaza katika historia ya Ligi ya Mabingwa barani ulaya. Mabao mawili ya mwanzoni mwa mchezo yalifungwa na Kasper Høgh na bao la pili kutoka kwa Jens Petter Hauge yaliwazidi wapinzani wao katika Uwanja wa Aspmyra. Rayan Cherki alipata […]

MOHAMED SALAH AREJEA LIVERPOOL

Mohamed Salah alirejea kwenye kikosi cha Liverpool, kufuatia kuwakilisha Misri kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika, huku klabu ikiendeleana  maandalizi ya mchezo wa Champions League dhidi ya Marseille. Salah, akiwa na tabasamu, alifanyiwa mazoezi katika kituo cha mafunzo cha klabu pamoja na wachezaji wengine wote wa Arne Slot kabla ya mchezo wa leo nchini Ufaransa. Kurudi kwa mshambuliaji […]

NG’ETICH NA EBENYO KUONGOZA SIRIKWA CLASSIC

Bingwa wa Dunia wa mbio za nyika, Agnes Ng’etich, na mshindi wa nishani ya fedha ya mita 10,000 kwenye Mashindano ya Dunia 2023, Daniel Ebenyo, wataongoza toleo la tano la Sirikwa Classic Cross Country Tour litakalofanyika Jumamosi, Februari 14 mwaka huu mjini Eldoret Nyota hao wawili wanatarajiwa kushiriki wakiwa bado kwenye kiwango bora kufuatia maonyesho yao […]

KAHATA AWEKA MATUMAINI KWA KCB

Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Gor Mahia, Francis Kahata, ameonyesha matumaini kuwa bao lake la kwanza litakuwa mwanzo wa mafanikio mema kwa klabu yake mpya huku nusu ya pili ya ligi ikianza. Kiungo huyo mkongwe alipachika bao wakati KCB iliposhinda Posta katika ushindi muhimu uliopatikana kwenye Uwanja wa Kasarani Bao hilo lilikuwa la kwanza la ligi […]

KIZZA BESIGYE AHAMISHWA HOSPITALINI KUFUATIA HALI MBAYA YA AFYA

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Dkt. Kizza Besigye, aliondolewa gerezani na kukimbizwa hospitalini baada ya afya yake kudorora na kufikia hali hatari usiku wa kuamkia Jumanne. Besigye, kiongozi wa PFF, amekuwa gerezani kwa muda na alipokuwa akikimbizwa hospitalini, msafara wake uliandamana na maafisa wengi wa usalama. Chama chake kimeshutumu serikali kwa kumnyima Besigye huduma bora […]

BABU OWINO AKANUSHA USHIRIKIANO NA GACHAGUA

Mbunge wa Embakasi Mashariki, Babu Owino, amekanusha madai kuwa anatafuta aliyekuwa Naibu Rais, Rigathi Gachagua, kwa lengo la kushirikiana naye kisiasa, huku akisisitiza kuwa nia yake ni kuchukua uongozi ndani ya chama cha ODM. Owino amesema lengo lake kuu ni kuvutia kura kutoka kwa jamii zote jijini Nairobi ili kutimiza azma yake ya kuwania ugavana, […]

OGAMBA AWAOMBA WAZAZI KURIPOTI SHULE ZINAZOKIUKA SHERIA

Waziri wa Elimu, Julius Ogamba, amewataka wazazi kuripoti shule zinazowalazimisha kununua sare au vifaa vya masomo kutoka kwa wauzaji maalum, akisisitiza kuwa hatua za kisheria zinaweza kuchukuliwa tu pale malalamishi yanapoungwa mkono na ushahidi. Wito huo unajiri huku malalamishi yakiongezeka kutoka kwa wazazi wa wanafunzi wa Gredi 10 kuhusu gharama kubwa ya sare za shule na madai […]