BUNGE KUANGAZIA UTEUZI WA NLC

Bunge linatarajiwa kuwapiga msasa watu 7 walioteuliwa na Rais William Ruto kuwa makamishna wa tume ya kitaifa ya ardhi, NLC, baada ya Rais Ruto kuwasilisha majina hayo bungeni. Saba hao ni pamoja na Dr Abdillahi Saggaf (Kwale) ambaye ameteuliwa kuwa mwenyekiti, wanachama wakiwa Susan Khakasa Oyatsi kutoka Kakamega, Daniel Murithi (Meru), Kigeni Vincent Cheruiyot (Kericho), […]

UHAMISHO WA MAJUKUMU YA KAUNTI YA NAIROBI

Serikali ya kaunti ya Nairobi kwa mara ya pili sasa imetia saini mkataba wa uhamisho wa majukumu kwa serikali kuu tangu kuanzishwa kwa ugatuzi nchini, tofauti na sasa mtindo utakaotumiwa kuongoza marekebisho jijini ukikosa kuwekwa wazi ikizingatiwa kuwa serikali za awali zilitumia mamlaka ya NMS. Kulingana na gavana wa Nairobi Johnson Sakaja, mchakato huo ni […]

MATUMAINI YA MAISHA MAPYA MAI MAHIU

Mamia ya familia zilizoachwa bila makao katika eneo la Mai Mahiu kutokana na bwawa kuvunja kingo zake na kusomba makazi yao mwaka 2024, zimepata tumaini la maisha mapya baada ya serikali kuzipa makazi mapya, ambapo kila mmiliki wa ardhi ameratibiwa kupokea ekari mbili za ardhi kama fidia. Naibu Rais Kithure Kindiki, aliongoza hafla ya kuzikabidhi […]

MBADI, WAZEE WA LUO WAKOSOA MALUMBANO ODM

Uongozi wa jamii ya Luo umehimiza mazungumzo kati ya mirengo kinzani ndani ya chama cha ODM, uongozi huo ukihofia uhasama kwenye chama hicho ikiwa miezi 4 tangu kifo cha kinara mwanzilishi marehemu Raila Odinga. Kwenye mkutano na Waziri wa fedha John Mbadi, baraza la wazee wa jamii hiyo limekosoa vuta nikuvute inayoendelea chama, huku Waziri […]

DOZI YA KWANZA YA PREP KUKABILI UKIWMI YAWASILI

Juhudi za serikali kukabili maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI zimepigwa jeki kufuatia kuwasili kwa shehena ya kwanza ya dozi 21,000 za dawa ya kinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa huo yaani PREP inayodungwa, dozi nyingine 12,000 zikitarajiwa kuwasili nchini mwezi Aprili. Shehena hiyo imewasilishwa kupitia ushirikiano kati ya serikali na shirika la Global Fund, dozi […]

MOURINHO APUUZILIA MBALI TETESI ZA MADRID

Kocha wa klabu ya Benfica, Jose Mourinho, amesema ana uwezo wa kusema hapana iwapo Rais wa Real Madrid, Florentino Perez, atamwendea, huku akipuuzilia mbali uvumi wa kurejea klabuni hapo. Kauli hiyo inajiri huku Benfica wakijiandaa kuwakaribisha Real Madrid katika mechi ya mchujo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, kabla ya marudiano yatakayochezwa wiki ijayo katika uga […]

MACHAKA AONA MAFUNZO BAADA YA SAFARI YA BARA

Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Nairobi United, Brian Machaka, amekiri kuwa safari ya timu hiyo katika Kombe la Shirikisho Afrika imefikia tamati, lakini akasema mafunzo waliyopata yatawajenga kumaliza vyema msimu wa ligi ya nyumbani. Machaka amesema kushiriki mashindano ya bara kumeibadilisha timu kifikra na kuinua viwango vya ndani, akiongeza kuwa kukabiliana na soka la Afrika […]

TUSKER WAMFUTA OKERE, MFARANSA ATEULIWA

Klabu ya Tusker FC imemtimua kocha mkuu Charles Okere kufuatia mfululizo wa matokeo yasiyoridhisha katika Ligi ya FKF, na kumteua kocha raia wa Ufaransa Julien Mette kuchukua mikoba hiyo. Shinikizo kwa Okere liliongezeka baada ya kipigo cha mabao 3–1 dhidi ya Mathare United, matokeo yaliyowaacha Brewers nafasi ya tisa wakiwa na pointi 28, tofauti ya pointi […]

OKWEMBA ATAKA SOKA LA KENYA LIBORESHWE

Aliyekuwa kiungo wa timu ya taifa ya Harambee Stars, Charles Okwemba, amelitaka Shirikisho la Soka Kenya kuboresha viwango vya soka ili kuifanya Kenya iwe shindani katika mashindano ya kimataifa. Kauli yake inajiri muda mfupi baada ya klabu ya Nairobi United kumaliza mkiani mwa Kundi B katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika bila pointi hata […]

WETANG’ULA ATETEA HAZINA YA NG-CDF

Spika wa Bunge la Kitaifa, Moses Wetang’ula, amesisitiza dhamira ya Bunge kulinda Hazina ya Maendeleo ya Maeneo Bunge, akisema ni rasilimali ya umma iliyolindwa kisheria. Wetang’ula amesema hazina hiyo inajibu moja kwa moja mahitaji ya wananchi katika maeneo bunge, ikichangia maendeleo ya miradi ya elimu, miundombinu na huduma za kijamii. Aidha, ameahidi kuwa Bunge litaendelea […]