AKIBA YA FEDHA ZA KENYA YAPANDA KWA SH 266BN CHINI YA EUROBOND

Akiba ya fedha za kigeni nchini Kenya imeongezeka hadi Sh1.88 trilioni, ikitoa malipo ya uagizaji bidhaa kwa miezi 6, kulingana na sasisho la hivi punde la Benki Kuu ya Kenya. Katika taarifa yake ya kila wiki, mdhibiti aMEsema hifadhi hizo zimesalia juu zaidi ya mahitaji ya kisheria ya angalau miezi minne ya bima ya kuagiza, […]

MSWADA WA KUDHIBITI MAZOEZI YA WASANIFU KUWASILISHWA BUNGENI

Sheria mpya inayotaka kuimarisha udhibiti wa taaluma ya usanifu na mafunzo ya viwango vya juu na utoaji wa leseni za watendaji imeanzishwa katika Bunge la Kitaifa. Mswada wa usanifu wa Majengo, 2026, unaofadhiliwa na Mbunge wa Bumula Wanami Wamboka, unapendekeza kubuniwa kwa taasisi mpya za kusimamia viwango vya kitaaluma, mafunzo, na usajili wa wasanifu majengo na mafundi wa usanifu majengo […]

DROO YA ROBO FAINALI YA FA CUP KUANDALIWA

Jumla ya timu 8 zinasubiri kufahamu wapinzani wao katika awamu ya robo fainali ya dimba la FA Cup nchini Uingereza baada ya kufuzu katika mechi zilizosakatwa Jumamosi na hapo jana. Manchester City walifuzu awamu hiyo baada ya kutoka chini na kuandikisha ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Newcastle United ugani St. James Park. Ushindi wao […]

KCB RFC, KABRAS RFC WAGAWANA HASARA YA MVUA

Klabu za raga KCB RFC na bingwa mtetezi Kabras RFC zililazimika kukubali sare ya 10-10 baada ya mechi kati yao kukatizwa na mvua nyingi iliyosababisha maji mengi katika uwanja wa KCB Sports Club Ruaraka. Mechi hiyo ya Kenya Cup iliyokuwa imewaleta pamoja miamba 2 wa raga ambao hawajapoteza mechi msimu huu, ilikuwa imepigiwa upato kuwa […]

BB BREAD YABOMOA GOR, AFC LEOPARDS

Timu ya BB Bread kutoka mtaani Kayole imesimamisha safari ya Gor Mahia kuelekea fainali za FKF Cup walikofika msimu jana na kupoteza kwenye fainali dhidi ya Nairobi United. Baada ya kuwabandua AFC Leopards katika Raundi ya 64, BB Bread iliibua mshtuko mwingine wa kuwabandua miamba wa soka, mara hii wakiicharaza Gor Mahia bao 1-0 katika […]

RUTO: TUTAONGEA NA ODM KWA USAWA

Rais William Ruto amesisitiza haja ya ushirikiano kati ya chama cha UDA na ODM kwenye uchaguzi mkuu ujao, akiwataka viongozi wa ODM kuwapuuza wanaopinga ushirikiano huo. Akizungumza katika kaunti ya Siaya, Ruto amesema mazungumzo baina ya vyama hivyo yataendeshwa kwa usawa kabla ya kuafikia ushirikiano. Amesema kuwa ripoti kuhusu ajenda 10 na ile ya NADCO […]

SAKAJA: MFUMO WA MAJITAKA FINYU

Gavana wa kaunti ya Nairobi Johnson Sakaja amekariri kuwa mfumo wa majitaka katika jiji la Nairobi hauwezi kuhimili kiwango cha mafuriko, hatua anayosema itatatuliwa kupitia kwa mkataba wa ushirikiano kati ya serikali yake na ile ya kitaifa. Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga, Sakaja amesisitiza kuwa mfumo wa mapato ya kaunti pekee hauwezi kutoa […]

MVUA YA MAANGAMIZI

Idadi ya watu waliofariki kutokana na mafuriko kote nchini imethibitishwa kufikia watu 42, huku familia zikiachwa na hasara kutokana na uharibifu wa mali yakiwemo mashamba, nyumba na magari. Takwimu za serikali zinaashiria kuwa zaidi ya familia 10,000 zimeathirika na mafuriko hayo, zaidi ya watu 4,000 wakilazimika kutafuta makazi katika maeneo salama. Hata hivyo, Waziri wa […]

MVUA KUPUNGUA ILA HATARI INGALIPO- UBASHIRI

Kiwango cha mvua inayonyesha nchini kimebashiriwa kupungua wiki hii ila hatari ya mafuriko itaendelea, wakenya wakitakiwa kuchukua tahadhari na kuhamia nyanda za juu. Kupitia taarifa, idara ya hali hewa imesema licha ya mvua kupungua, ardhi nyingi haziwezi kustahimili maji zaidi kutokana na mvua kubwa katik wiki za hivi karibuni, na hivyo manyunyu pekee yanaweza kusababisha […]

Online Blackjack in Maryland: Where Luck Meets Regulation Deposit limits and self‑exclusion tools protect users in online blackjack maryland (MD): casinos-in-maryland.com. Maryland’s name has long been linked to Washington, D. C., but lately it’s also become a hub for digital gambling. In 2023, the state’s online blackjack market jumped 17% – the biggest rise among […]