OGAMBA: KUNA NAFASI YA KUBADILISHA SHULE

Wazazi walio wa wanafunzi wanaojiunga na gredi ya 10 wamepewa hakikisho kwamba wangali na nafasi ya kubadilisha shule walizowekwa wanao, baada ya kuibuka kwamba baadhi ya wanafunzi wamewekwa katika shule za jinsia tofauti. Hakikisho hilo limetolewa na Waziri wa Elimu Julius Ogamba, huku zoezi la kuwapokea wanafunzi hao likiingia siku ya pili hii leo baada […]

JSC YAENDELEZA MSAKO WA MAJAJI

Mwenyekiti wa mamlaka ya kuangazia utendakazi wa polisi IPOA Issak Hassan na mchanganuzi wa masuala ya kikatiba Prof Migai Aketch, ni miongoni mwa wawaniaji wanaotaka kuteuliwa kama majaji wa mahakama ya rufaa kwenye mchakato unaoendelea wa kuwateua majaji wa mahakama hiyo na mahakama kuu. Akizungumza mbele ya jopokazi la uteuzi la tume ya JSC, Hassan […]

HATIA MASHIRIKA YA UMMA KUTUMIA HUDUMA ZA BINAFSI- MAHAKAMA

Mahakama kuu imetoa amri za muda kuzuia mashirika ya umma kuwakilishwa mahakamani na mawakili binafsi hadi kesi ya kikatiba iliyowasilishwa na seneta wa Busia Okiya Omtatah, mkenya kwa jina Dakta Benjamin Magare na wengine itakaposikilizwa na kuamuliwa. Katika uamuzi huo, mahakama aidha imemwagiza mdhibiti wa bajeti ya serikali kutoidhinisha malipo yoyote kwa mawakili wasio wa […]

NCA YADAI JENGO HALIKUWA LIMESAJILIWA

Imebainika kwamba jengo lililoporomoka mtaani Karen jijini Nairobi Jumamosi iliyopita halikuwa limesajiliwa inavyohitajika kisheria. Haya ni kulingana na mamlaka ya kitaifa inayosimamia mijengo NCA, ikisema kuwa uchunguzi wa awali umeashiria dosari katika muundo wa jengo hilo la ghorofa moja lililoporomoka kutokana na uzito wa zege. Watu wawili walifariki, wawili wakapata majeraha mabaya huku wengine 7 […]

MASAIBU YA UNITED YAZIDI KIWANGO

Masaibu yameendelea kurundika uga wa Old Trafford baada ya Manchester United kupewa kichapo cha mabao 2-1 na Brighton na hivyo kubanduliwa nje ya kombe la FA katika raundi ya 3 hapo jana, ikiwa ni mara ya kwanza kwa United tangu msimu wa 1981-82 kubanduliwa nje ya Carabao Cup na FA Cup katika awamu za mwanzo. […]

AFCON 2025: NDIDI AKOSA NUSU FAINALI DHIDI YA MOROCCO

Timu ya taifa ya Nigeria, Super Eagles, itamkosa nahodha wao Wilfred Ndidi katika nusu fainali dhidi ya Morocco baada ya kiungo huyo kusimamishwa kwa mechi moja. Ndidi alipata kadi yake ya pili ya njano katika mashindano hayo wakati wa ushindi wa mabao 2–0 dhidi ya Algeria, jambo lililosababisha adhabu ya kusimamishwa moja kwa moja kwa mechi moja. Awali […]

REGRAGUI APINGA VIKALI MADAI YA UPENDELEO WA WAAMUZI KWA MOROCCO

Kocha wa timu ya taifa ya Morocco, Walid Regragui, amepinga kwa hasira madai kwamba timu yake inanufaika na maamuzi ya upendeleo kutoka kwa waamuzi kama wenyeji wa Kombe la Mataifa bingwa barani Afrika (AFCON) 2025. Atlas Lions wanatarajiwa kukutana na vigogo wenzao Nigeriakatika nusu fainali kali itakayochezwa Jumatano, Regragui akishikilia kuwa faida ya pekee walio nayo ni kucheza mbele ya mashabiki 65,000 […]

SSENYOJO AWAHAKIKISHIA CHUI WINDO LA KPL

AFC Leopards waliharibika na kuvunja vibuyu vya Tusker FC ugani Nyayo, kwa kuwatandika kichapo cha mabao 4-0 kwenye mechi ya ligi kuu KPL na kuongeza mwanya wa uongozi. Mganda Samuel Ssenyonjo aliwapa Ingwe uongozi wa mabao 2-0 kabla ya kutamatika kwa kipindi cha kwanza, Robert Sichenje akafunga la 3 na kisha Ssenyonjo akarejea kukamilisha hattrick […]

OWALO AJIUZULU

Naibu mkuu wa wafanyakazi wa Ikulu anayesimamia kitengo cha ufanikishaji wa utendakazi wa serikali ya Kenya Kwanza Eliud Owalo, amejiuzulu baada ya kutangaza azma yake ya kuwania urais kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka ujao. Kupitia taarifa, Owalo amesema haiwezekani kwake kuendelea kuitumikia serikali ya Rais William Ruto baada yake kutangaza kuwania wadhifa huo. Kulingana na […]

MATIANG’I ASHINIKIZA MAGEUZI YA ELIMU

Aliyekuwa Waziri wa usalama Fred Matiang’i, amehimiza haja ya vikao vya dharura kuandaliwa ili kujadili na kupata suluhu kwa changamoto zinazoikabili sekta ya elimu nchini. Akizungumza kwenye kaunti ya Kiambu, Matiang’i ambaye ni naibu kinara wa chama cha Jubilee, amesisitiza haja ya sekta hiyo kufanyiwa mageuzi ili kuilainisha. Aidha, amekosoa madai kwamba serikali imeingiza siasa […]