SESKO ATALETA MWANGA, FLETCHER

Kocha mshikilizi wa Manchester United Darren Fletcher ana matumaini kwamba mabao mawili yaliyofungwa na Benjamin Sesko katika sare ya mabao 2-2 dhidi ya Burnley jana usiku ni kiashiria cha kuimarika kwake baada ya kipindi kigumu kwa raia huyo wa Slovenia. Sesko alikuwa amefunga mara 2 pekee katika mechi 17 kabla ya jana tangu kuwasili kwake […]

GUARDIOLA APOTEZA TUMAINI EPL

Kocha mkuu wa Manchester City Pep Guardiola amekiri kuwa klabu hiyo haiwezi kufikiria kuipata Arsenal kileleni mwa ligi katika kinyanga’nyiro cha kusaka ubingwa wa ligi hiyo msimu huu baada ya msururu wao wa sare kufikia mechi 3 mfululizo. Licha ya Erling Haaland kuwaweka City kifua mbele kakatika kipindi cha kwanza jinsi ilivyofanyika dhidi ya Chelsea, […]

LEOPARDS WAREJEA UONGOZINI KPL

Miamba wa soka nchini AFC Leopards wamerejea uongozini mwa ligi kuu ya soka KPL kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Nairobi United ugani Nyayo, na kupanda juu ya washikilizi wa rekodi ya ubingwa Gor Mahia kwa pointi 1. Naibois walijifunga bao kunako dakika ya 20 kabla ya Ingwe kufunga bao la pili kunako dakika […]

TRUMP: NITAIENDESHA VENEZUELA

Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuwa serikali yake itamwelekeza kikamilifu cha kufanya kiongozi wa muda wa Venezuela Delcy Rodriguez, ukiwemo uuzaji wa mafuta kwa muda usiojulikana baada ya kumbandua Nicolas Maduro. Kauli ya Trump inajiri huku Delcy akina kwamba hakuna utawala wan je unaoeindesha Venezuela Hata hivyo, Trump amesema Marekani italiendesha taifa hilo la […]

WANAFUNZI TRANS MARA SOUTH SHULENI

Hatimaye wanafunzi katika shule ya Sitet Comprehensive eneo la Trans Mara South wamepata fursa ya kurejea shuleni kwa muhula wa kwanza baada ya maafisa wa usalama kuwaondoa watu waliokuwa wakiishi kwenye shule hiyo. Operesheni hiyo iliongozwa na chifu wa Olodonyo-Orok Paul Rutto, mkurugenzi wa elimu eneo hilo George Muchina akiripoti kuwa wanafunzi wapatao 250 waliripoti […]

DUALE, KUCO WAKOSA MWAFAKA

Huenda wakenya wakaendelea kuhangaika kupata matibabu kutokana na mgomo wa maafisa wa kliniki unaoendelea kutokana na mvutano kati ya viongozi wa muungano wa maafisa hao KUCO na Waziri wa afya Aden Duale, ambaye amedinda kutia saini mkataba wa maelewano ya kurejea kazini ulioidhinishwa na tume ya kuratibu mishahara ya wafanyakazi wa umma SRC. Kwa mujibu […]

UPINZANI WADAI NJAMA YA UDANGANYIFU 2027

Muungano wa upinzani umeibua madai ya kuwepo kwa njama ya kuiba kura kwenye uchaguzi mkuu ujao kupitia kampuni ya Smartmatic iliyotoa huduma za teknolojia kwenye vyombo vya dijitali vya uchaguzi wa mwaka wa 2022, ikitaka kandarasi ya kampuni hiyo ifutiliwe mbali. Kulingana na viongozi wa upinzani akiwemo kinara wa DCP Rigathi Gachagua, Kalonzo Musyoka wa […]

RUTO AWAPOTOSHA WAKENYA, MUSYOKA

Rais William Ruto analenga kutumia ajenda ya kuibadilisha Kenya kuwa mfano wa taifa la Singapore kuwapotosha wakenya na kuvuruga fikra zao ili wakose kumwajibisha kuhusiana na utendakazi wake. Haya ni kulingana na makamu wa zamani wa Rais Kalonzo Musyoka na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua, wakisema haifai kulinganisha Kenya na taifa jingine. Walikuwa wakizungumza kwenye […]

FATAKI ZA EPL

Manchester City watalenga kupunguza mwanya wa pointi kati yao na viongozi wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza Arsenal, watakapoikaribisha Brighton ugani Etihad leo usiku. City ambao walipoteza pointi 4 katika mechi 2 zilizopita, watakosa huduma za mabeki wao mahiri Ruben Diaz na Josko Gvardiol kutokana na majeraha, City wakilalizimika kumrejesha beki wao Max Alleyne […]

DIALLO ANG’AA KWA IVORY COAST

Kiungo wa Manchester United Amad Diallo alikuwa nyota mchezoni jana usiku wakati mabingwa watetezi wa dimba la taifa bingwa barani Afrika AFCON 2025 Ivory Coast waliwadhalilisha Burkina Faso kwa kibano cha mabao 3-0 kwenye awamu ya mwondoano, Ivory Coast wakiwa mabingwa watetezi wa kwanza wa AFCON kufika awamu ya robo fainali tangu mwaka wa 2010. […]