AFC LEOPARDS WATOA KUCHA HUKU K’OGALO WAKISUA UBINGWA

AFC Leopards wameimarisha nafasi yao katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Sportpesa kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Murang’a Seal katika Uwanja wa Nyayo Jumapili, wakikaribia kufikia viongozi na wapinzani wao wakali, Gor Mahia. Mchezo ulianza kwa tahadhari kubwa na wasiwasi chini ya jua la Nairobi, lakini baada ya mapumziko, Ingwe walipata midhihirisho […]

SHUJAA WAJIANDAA KWA FAINALI ZA HONG KONG SEVENS

Kikosi cha shujaa, kikiwa na makamu wa nahodha Samuel Asati, kinaamini kuwa uthabiti wa akili na kuboresha ujuzi msingi wa michezo itakuwa muhimu wakati Shujaa wanapojiandaa kwa Michuano ya Dunia ya Hong Kong Sevens ndani ya wiki mbili zijazo. Timu hiyo ina muda mfupi wa maandalizi, baada ya kurejea nchini Alhamisi na kuanza mazoezi kesho. Kocha mkuu, Kevin Wambua, ameweka msisitizo […]

SENEGAL YAPIGA MARUFUKU SAFARI ZISIZO ZA LAZIMA

Serikali ya Senegal imewapiga marufuku mawaziri wake kufanya safari za nje zisizo za lazima kufuatia kupanda kwa bei ya mafuta kutokana na mgogoro wa Mashariki ya kati. Akizungumza katika mkutano wa vijana Waziri Mkuu Ousmane Sonko amesema kuwa gharama ya pipa la mafuta imekaribia mara mbili ya kiwango kilichokuwa kimepangwa kwenye bajeti. Sonko ameahirisha safari zake […]

VITUO 30 VYA AFYA KUSHTAKIWA KWA ULAGHAI WA SHA

Wamiliki na wakurugenzi wa vituo 30 vya afya wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za ulaghai iwapo Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma atatoa idhini ya mashtaka hayo. Kurugenzi ya Upelelezi wa Jinai imesema uchunguzi wa malalamishi ya ulaghai pamoja na ukaguzi wa kitaalamu wa miamala ya vituo hivyo umebaini kuwa wote wana kesi ya kujibu. Tayari […]

UHURU AKOSOLEWA NA VIONGOZI WA ODM

Rais mstaafu Uhuru Kenyatta anaendelea kukosolewa kufuatia kauli alizotoa katika kaunti ya Kirinyaga wiki iliyopita, alipowahimiza Wakenya kufanya maamuzi bora na yenye ufahamu katika uchaguzi ujao. Viongozi wa mrengo wa Linda Ground ndani ya chama cha ODM ndio wa hivi punde kumkosoa, wakimtuhumu kujihusisha na siasa za mgawanyiko. Chama hicho pia kimesisitiza kuwa mgawanyo wa maeneo utakuwa miongoni mwa […]

KINDIKI AWAHIMIZA WAKENYA KUJISAJILI KAMA WAPIGA KURA

Naibu Rais, Kithure Kindiki, amewataka Wakenya ambao bado hawajasajiliwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika orodha ya wapigakura kabla ya muda uliowekwa kukamilika. Kindiki amesema kuwa wale watakaoshindwa kujiandikisha hawatakuwa na uwezo wa kuchagua viongozi wanaowataka katika uchaguzi ujao. Akizungumza katika kaunti ya Tharaka Nithi, wakati wa sherehe za Pasaka, Naibu Rais amewahimiza wananchi kuchukua hatua mapema ili kushiriki kikamilifu […]

RUTO AONYA MAFISADI WA MAFUTA

Rais William Ruto ameonya kuwa wahusika wa mtandao wa ulanguzi katika sekta ya mafuta na petroli watakaotumia mgogoro wa Mashariki ya Kati kujinufaisha watakabiliwa na adhabu kali. Rais amesema serikali haitaruhusu watu wachache kutumia hali ya mgogoro huo kuwanyanyasa Wakenya kupitia vitendo vya ufisadi katika sekta ya mafuta. Akizungumza katika eneo bunge la Kilgoris, kaunti […]

NAIROBI KUKOSA MAJI KWA SIKU TANO KUANZIA LEO

Wakazi wa Nairobi wanatarajiwa kukumbwa na ukosefu wa maji kwa muda wa siku tano kuanzia leo kufuatia kusimamishwa kwa muda kwa mfumo muhimu wa usambazaji wa maji ili kuruhusu kazi za miundombinu. Kupitia taarifa kwa umma, Kampuni ya Maji na Majitaka ya Nairobi imetangaza kuwa Wakala wa Maendeleo ya Maji ya Athi utazima kwa muda mfumo wa […]

MJADALA WAIBUKA KUHUSU USHIRIKIANO KATI YA ODM NA UDA

Rais William Ruto anakabiliwa na mjadala kuhusu mustakabali wa baadhi ya wandani wake wa kisiasa, huku ODM ikisisitiza kuwa inalenga nafasi ya Naibu wa Rais. Katika kongamano la wajumbe wa chama hicho lililofanyika wiki jana, chini ya uongozi wa Oburu Oginga, ODM ilieleza umuhimu wa kuwa na makubaliano ya kina na chama cha UDA ili kuepuka tofauti iwapo pande […]

LIVERPOOL KUKUTANA NA MANCHESTER CITY FA CUP

Liverpool wanakabiliana na safari ngumu kwenda Manchester City katika mchezo wa FA Cup robo fainali, huku Mohamed Salah akitafuta kumalizia misimu tisa ya kuvutia Anfield kwa mafanikio. Arsenal na Chelsea wanatarajia kufika nusu fainali Wembley dhidi ya wapinzani wa ngazi ya chini. Wakati huo huo, West Ham na Leeds wamesitisha harakati zao za kuokoa nafasi […]