SHUJAA WAREJEA NCHINI KUTOKA BRAZIL

Timu ya taifa ya raga ya wanaume ya wachezaji 7 kila upande, Shujaa, imerejea nchini kutoka Sao Paulo Brazil ambako walitia for a katika mkondo wa mwisho wa HSBC SVNS II, na kufuzu awamu ya mabingwa. Shujaa ilimaliza katika nafasi ya 3 katika mikondo miwili ya kwanza iliyoandaliwa Kenya na Uruguay, kabla ya kuhitimisha kampeni […]

KIKOSI CHA HANDIBOLI MUSINGU CHALENGA KUKATA KIU CHA TAJI

Huku shule za upili zikijiandaa kwa michezo ya kitaifa kwa muhula wa kwanza, kikosi cha handiboli cha shule ya Musingu Boys kinalenga kutwaa tena taji la mchezo huo baada ya ukame wa miaka 15. Michezo hiyo itakayoandaliwa jijini Kisumu, itaanza tarehe 7 na kukamilika tarehe 11. Taji la handiboli limeikwepa shule hiyo kwa miaka 15, […]

FAMILIA ZA WAATHIRIWA VITA URUSI ZALIA

Imeibuka kwamba familia za wakenya waliouawa kwenye mapigano kati ya Urusi na Ukraine wamepewa chaguo kukubali jamaa zao wazikwe nchini Urusi au miili yao ichomwe kisha watumiwe majivu. Kulingana na familia hizo, idara inayosimamia wakenya walioko ughaibuni imezitaka kukubali jamaa zao wazikwe kwa heshima zote za kijeshi, au kuteketeza miili na kufanikisha usafirishaji wa majivu, […]

ODM YAANZISHA MCHAKATO WA KUMTIMUA SIFUNA

Katibu mkuu wa ODM Edwin Sifuna ana siku 4 kupinga kutimuliwa kwake kutoka wadhifa huo huku akitakiwa kufika mbele ya kamati ya nidhamu ya chama hicho tarehe 10 mwezi huu. Kupitia waraka uliotiwa saini na mwenyekiti Gladys Wanga, ODM imemtuhumu Sifuna na mashtaka 5, ikiwemo madai ya kukiuka msimamo wa chama kuhusu ushirikiano na UDA, […]

UHABA WA MAFUTA WANUKIA

Serikali imejiandaa kuwalinda wakenya dhidi ya bei ghali ya mafuta kutokana na uhaba wa bidhaa hiyo unaotarajiwa kufikia katikati mwa mwezi huu, ikisema itatumia takribani shilingi bilioni 17 kutoka hazina ya udhibiti wa bei kuwakinga wakenya dhidi ya bei ya juu ila kwa kipindi kifupi. Akiwa mbele ya kamati ya bunge la kitaifa kuhusu fedha […]

UPINZANI, SERIKALI WAVUTANA KUHUSU UBOMOAJI GIKOMBA

Vuta nikuvute baina ya serikali na muungano wa upinzani imeendelea kuhusu mpangilio mpya wa soko la Gikomba jijini Nairobi, muungano wa upinzani sasa ukiwataka wafanyabiashara sokoni humo kupinga kuhamishwa. Wakiongozwa na kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka, viongozi wa upinzani wamedai kuna njama ya kunyakua ardhi ya soko hilo kwa kuwahamisha wafanyabiashara, huku serikali ikisema inawahamisha […]

UJUMBE WA RUTO KUHUSU PASAKA

Huku Wakristo kote ulimwenguni wakiadhimisha siku kuu ya Pasaka, Rais William Ruto amewatakia Pasaka njema huku akiwahimiza kuitumia kutafakari kuhusu mwanzo mpya maishani mwao. Kupitia kanda fupi ya video aliyoichapisha kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii, Ruto amesema kipindi cha Pasaka ni mwanzo mpya miongoni mwa familia za wakenya na kuwataka kuliombea taifa. Amewataka […]

NTSA YATAKA KESI YA FAINI KUTUPILIWA MBALI

Mamlaka ya Kitaifa ya Usalama Barabarani, NTSA, imeiomba Mahakama Kuu kutupilia mbali kesi inayopinga utekelezaji wa mfumo wa faini za papo hapo, ikisema suala hilo limepitwa na wakati. Katika hati ya kujibu, mkurugenzi mkuu wa NTSA, Odhiambo Kondiwa, amesema mamlaka hiyo ilisitisha rasmi mpango huo Machi 27 mwaka huu hivyo kesi hiyo haina msingi wa kuendelea kusikilizwa. Kesi […]

MOTO WATEKETEZA NYUMBA ZA MAGEREZA LANG’ATA

Idara ya magereza nchini imethibitisha kuwa moto umeteketeza nyumba 30 za makazi ya maafisa katika Gereza la Wanawake la Lang’ata lenye ulinzi mkali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na idara hiyo moto huo ulizuka Jumatano jioni majira ya saa moja na nusu na kuteketeza nyumba hizo kabisa. Hata hivyo, idara hiyo imesema hakuna mtu aliyepoteza maisha au kujeruhiwa, huku […]

SERIKALI KUTOA VITAMBULISHO KUANZIA SHULE YA UPILI

Katibu wa Idara ya Uhamiaji na Huduma za Wananchi, Belio Kipsang, ameongoza zoezi la kuwahamasisha machifu kuhusu mwongozo mpya wa kuwasajili Wakenya waliofikisha miaka 18 kupata vitambulisho vya kitaifa. Zoezi hilo lililoanza mwezi Julai mwaka jana katika kaunti 20 limewezesha usajili wa watu milioni 1.7 hadi sasa, huku Kipsang akisema waombaji watapata vitambulisho ndani ya […]