MAGUIRE AENDELEZA MKATABA MANCHESTER UNITED

Nahodha wa zamani wa Manchester United, Harry Maguire, amesaini mkataba mpya wa mwaka mmoja na klabu hiyo, ukiwemo uwezekano wa kuongeza mwaka mwingine. Maguire mwenye umri wa miaka 33, ambaye mkataba wake wa sasa ungeisha mwishoni mwa msimu huu, aliungana na Manchester United kutoka Leicester City mwaka 2019 kwa kiasi cha pauni milioni 80, rekodi ya dunia […]

BAJABER AREJEA KIKOSI CHA TAIFA

Mchezaji wa Simba, Mohammed Bajaber, ameahidi kurejesha imani aliyopewa baada ya kuitwa tena katika kikosi cha taifa cha Harambee Stars kufuatia kipindi kigumu alichopitia kutokana na majeraha. Kiungo huyo mshambuliaji mwenye umri wa miaka ishirini na mitatu amerejea kikosini kwa mara ya kwanza baada ya takriban mwaka mmoja, akisema kuwa kipindi hicho kilimjaribu sana kimwili […]

MIDEVA AWANIA KIATU CHA DHAHABU

Mshambuliaji wa Ulinzi Starlets, Elizabeth Mideva, ameonyesha dhamira ya dhati ya kunyakua tuzo ya mfungaji bora katika msimu huu wa Ligi Kuu ya Wanawake nchini. Mideva, aliyewahi kusoma katika Shule ya Upili ya Wasichana ya Bishop Njenga, aliibuka nyota mwishoni mwa wiki alipofunga mabao matatu katika ushindi wa mabao matatu kwa moja dhidi ya mabingwa wa zamani […]

AJALI YA TRENI UFARANSA – MTU MMOJA AFARIKI

Dereva wa treni ya abiria ya mwendo wa kasi amefariki baada ya treni hiyo kugongana na lori lililokuwa limebeba vifaa vya kijeshi katika kivuko cha reli nchini Ufaransa. Watu kadhaa wamejeruhiwa katika ajali hiyo iliyotokea kati ya miji ya Béthune na Lens katika eneo la Pas-de-Calais kaskazini magharibi mwa nchi hiyo. Kwa mujibu wa taarifa, […]

TUNATAKA PAWA: WALIMU WA JSS WASHINIKIZA SERIKALI

Walimu wa shule za sekondari msingi katika kaunti ya Taita Taveta wameungana na wenzao kote nchini kushinikiza serikali kuangazia ajira ya kujisimamia pamoja na kupewa mikataba ya kudumu. Walimu hao wamelalamikia uongozi wa shule za msingi wakisema hauzingatii mahitaji ya sekondari msingi, wakidai wanakandamizwa chini ya usimamizi huo usioelewa mfumo wao wa ufundishaji. Aidha, baadhi […]

WALINZI WAWILI WAUAWA SANG’ALO – BUNGOMA

Hali ya taharuki imetanda katika eneo la Sang’alo, kaunti ya Bungoma, baada ya walinzi wawili kuvamiwa na watu wanaoshukiwa kuwa wahalifu. Kwa mujibu wa kamanda wa polisi wa Bungoma Kaskazini, William Letting, mmoja wa walinzi hao alipoteza maisha papo hapo huku mwenzake akiaga dunia alipokuwa akipokea matibabu hospitalini. Wakaazi wa eneo hilo wamelalamikia kuongezeka kwa […]

KICD YAAGIZA TAKWIMU ZA WANAFUNZI WA GREDI YA 10

Taasisi ya Ukuzaji Mitaala nchini imeagiza wakuu wa shule zote za umma za upili kuwasilisha takwimu za wanafunzi wa Gredi ya kumi ili kuandaa hatua inayofuata ya ugavi wa vitabu vya masomo. Mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo, Charles Ng’ondo, amekiri kuwepo kwa mapungufu ambapo baadhi ya shule zina vitabu vingi kupita kiasi huku nyingine zikiwa hazijapokea hata […]

ODM NA UDA ZAZOZANA KISIASA ENEO LA NYANZA

Vyama vya ODM na UDA vimeingia katika mvutano mkali kuhusu msimamo wa ODM wa kutaka chama tawala kisiwasilishe wagombeaji katika maeneo inayodai kuwa ngome zake. Viongozi wa ODM wanamtaka Rais William Ruto pamoja na Seneta wa Siaya Dkt Oburu Oginga kuingilia kati suala hilo mapema ili kuepusha mgawanyiko zaidi wa kisiasa. Kwa upande wake, ODM […]

SEKTA YA MAJANI CHAI YAONYESHA UKUAJI – KENYA

Sekta ya majani chai nchini imeonyesha ukuaji kwa kiasi kikubwa, ikiandikisha thamani ya Shilingi bilioni 218.79 sokoni katika bajeti ya mwaka uliopita. Hata hivyo, Ukuaji huo umehusishwa na mikakati thabiti ya mauzo na mageuzi yanayoungwa mkono na serikali ambayo yamepanua soko la Kenya kimataifa kutoka masoko 96 hadi 100 ya kuuza mazao ng’ambo. Kufuatia ripoti ya Utendakazi wa […]

UTABIRI WAONYESHA MVUA KUENDELEA

Wakazi walio katika nyanda za juu za eneo la kati mwa nchi, Magharibi na mwambao wa pwani wametahadharishwa kuhusu kubwa itakayoendelea katika kipindi cha kuanzia leo hadi Jumatatu wiki ijayo. Kwenye ubashiri wake wa wiki moja, idara ya utabiri wa hali ya anga imesema manyunyu pia yanatarajiwa katika baadhi ya maeneo ya South Rift, nyanda […]