OGAMBA: SERIKALI IMETATUA DENI LA WACHAPISHAJI VITABU

Waziri wa Elimu Julius Migos Ogamba amesema serikali imetatua mzozo wa deni la wachapishaji vitabu, hatua inayofungua upya mchakato wa uchapishaji na usambazaji wa vitabu shuleni. Ogamba amesema Wizara ya Fedha imetoa shilingi bilioni tano nukta sita, fedha zitakazowezesha kuendelezwa kwa shughuli za uchapishaji zilizokwama kwa muda. Waziri huyo ameongeza kuwa Wizara ya Elimu inatarajiwa […]

WANAOHODHI MAFUTA CHUMA MOTONI

Mamlaka inayodhibiti ushindani wa kibiashara nchini imezionya kampuni za uuzaji wa mafuta nchini dhidi ya kuficha mafuta hayo kwa matarajio ya kuuza kwa bei ya juu kutokana na uhaba unaoendelea kuripotiwa nchini. Kupitia taarifa, mamlaka hiyo imesema ina ufahamu kuhusu mjadala unaoendelea kuhusu uwepo wa mafuta ya petroli, diseli, mafuta ya taa na ndege kote […]

KESI MAHAKAMANI IKITAKA WANDAYI NJE

Kesi imewasilishwa katika mahakama kuu ya Milimani ikitaka kutimuliwa kazini Waziri wa kawi Opiyo Wandayi kuhusiana na Sakata ya uagizaji wa mafuta yanayodaiwa kuwa chini ya viwango hitajika nchini. Mlalamishi kwa jina Francis Owino ameitaka mahakama kuorodhesha kesi hiyo kama ya dharura na kutoa amri ya kumzuia Wandayi dhidi ya kutekeleza majukumu yake kama Waziri […]

MBUNGE KIARAHO KUZIKWA IJUMAA

Mbunge wa Ol Kalou David Kiaraho ameratibiwa kuzikwa hii leo katika eneo la Tigoni kaunti ya Kiambu ambako hafla ya mazishi inaendelea. Naibu Rais Kithure Kindiki ni miongoni mwa viongozi wakuu serikalini wanaohudhuria hafla ya mazishi ya mbunge huyo ambaye ameombolezwa kama mvumilivu na mwenye bidi. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

NAIROBI KUPATA SURA MPYA 

Jiji la Nairobi limeratibiwa kupata mwonekano mpya kufuatia kutia saini kwa makubaliano ya kuanzisha kwa ukumbi wa kisasa wa michezo na burudani katika eneo la reli katikati mwa jiji, ambao umeratibiwa kukamilika ndani ya miezi 12 ijayo. Mradi huo utakaogharimu mabilioni ya pesa unalenga kuipa kaunti ya Nairobi sura mpya na kuiwezesha kushindana na miji […]

KENYA YAANGAZIA MAUZO YA KWENDA CHINA KWA KASI KABLA YA KUONDOLEWA USHURU

Matarajio yanaongezeka kote katika sekta ya kilimo ya nje ya Kenya huku Uchina inapojitayarisha kutekeleza sera ya kutotoza ushuru kwa bidhaa mbalimbali za Afrika kuanzia Mei 1. Kwa wengi, hiyo ni hatua isiyokuwa ya kawaida ambayo wauzaji bidhaa nje wanasema inaweza kufafanua upya mtiririko wa biashara kati ya bara na uchumi wa pili kwa ukubwa duniani. […]

LIGI KUU YA SOKA UINGEREZA EPL YAREJEA

Ligi kuu ya soka nchini Uingereza, EPL, itarejea wikendi hii baada ya kuchukua mapumziko ya wiki 3 kuwaruhusu wachezaji kuwajibikia timu zao za taifa na awamu ya robo fainali ya kombe la FA. Yanayoangaziwa pakubwa ni timu kuwania nafasi za kucheza barani Ulaya msimu ujao, mbali na kinyang’anyiro kati ya Arsenal na Manchester City kuwania […]

VILLA GUU MOJA SEMI FAINALI UROPA LEAGUE

Klabu ya Aston Villa itaingia katika mkondo wa pili wa mechi ya robo fainali ya dimba la UROPA League ikiwa na uongozi wa mabao 3-1 kufuatia ushindi wao hapo jana kwenye mechi ya mkondo wa kwanza dhidi ya Bologna nchini Italia. Baada ya kuponea awimbi ya mashambulizi kutoka kwa wenyeji wao, Villa walichukua uongozi kupitia […]

KSSSA: LAISER HILL KUVAANA NA FSK KWENYE VIKAPU

Mabingwa watetezi wa mchezo wa vikapu wa wavulana katika michezo ya shule za upili Laiser Hill, watachuana na Friends School Kamusinga hii leo katika semi fainali za mashindano ya shule za upili kwa muhula wa kwanza jijini Kisumu. Laiser Hill walipata ushindi mwembamba dhidi ya Lukenya School wa 71-69 na kuweka miadi ya kumenyana na […]

WASHTAKIWA KWENYE KESI YA MUCHAI WAHUKUMIWA KIFO

Washtakiwa wanne waliohusishwa na mauaji ya aliyekuwa mbunge wa Kabete George Muchai mnamo mwaka wa 2015, wamepewa hudukumu ya kifo huku wenzao wawili wakihukumiwa kifungo cha miaka 10 gerezani kila mmoja. Hakimu mkuu Lucas Onyina, alitoa uamuzi huo hapo jana baada ya kuwapata 6 hao na hatia ya mashataka kadhaa ikiwemo wizi wa kimabavu na […]