AFC LEOPARDS YASAKA KUJIKWAMUA DHIDI YA NAIBOIS

Miamba wa soka nchini AFC Leopards watashuka uwanjani hii leo dhidi ya Nairobi United, Leopards maarufu kama Ingwe wakilenga kuweka kando masaibu yao na kuonyesha mwamko mpya. Ingwe wataingia uwanjani leo wakiwa na majeraha ya kichapo cha mabao 4-1 dhidi ya Mathare United wikendi iliyopita, kichapo kilichodidimiza matumaini ya kunyakua taji la ligi kuu ya […]

MUDAVADI: HAKUNA FIDIA KWA WAATHIRIWA WA URUSI

Wakenya waliouawa au kujeruhiwa katika vita kati ya Urusi na Ukraine hawatapewa fidia na serikali, na badala yake serikali itawasaidia wanaotaka kurejea nchini kufanya hivyo. Akizungumza jijini Moscow, Urusi, Mkuu wa Mawaziri Musalia Mudavadi, amepuzilia mbali uwezekano wa serikali kuwapa fidia wakenya hao, akisisitiza msimamo wa Urusi kwamba walijitolea kupigana katika vita hivyo. Familia za […]

MATUSI YA VIONGOZI YASHANGAZA TAIFA

Maswali yameibuka kuhusu ukiukaji wa sura ya 6 ya katiba kuhusu maadili miongoni mwa viongozi wakuu serikalini, kufuatia hatua ya viongozi hao akiwemo Rais William Ruto na aliyekuwa naibu wake Rigathi Gachagua kurushiana matusi hadharani kuhusu mwonekano na masuala ya kibinafsi. Wawaili hao wamekuwa wakirushiana matusi katika siku za hivi karibuni, wakenya wakijiuliza iwapo viongozi […]

MVUA KUBWA KUANZA ALHAMISI

Wakenya wametahadharishwa kuhusu viwango vya juu vya mvua katika baadhi ya maeneo tya nchi kuanzia hapo kesho, idara ya utabiri wa hali ya anga ikisema mvua hiyo itanyesha kwa vipindi. Kwa mujibu wa utabiri wake, nyanda za juu za magharibi na mashariki mwa bonde la ufa, ukanda wa Ziwa Victoria, nyanda za chini za Mashariki […]

SAKAJA: WAFANYABIASHARA WA GIKOMBA SHARTI WAHAME

Serikali ya kaunti ya Nairobi imekariri kuwa wafanyabiashara wote walio ndani ya umbali wa mita 50 kutoka Mto Nairobi katika soko la Gikomba ni sharti wahame licha ya pingamizi hapo jana, ikisema wametengewa sehemu mbadala sokoni humo kwa muda ujenzi wa soko jipya unapoendelea. Zoezi la kutathmini umbali huo hapo jana lilisitishwa ghafla baada ya […]

KIVUMBI UCL: REAL MADRID vs MAN CITY, CHELSEA vs PSG

Kivumbi kinatarajiwa kushuhudiwa hii leo katika michuano ya klabu Bingwa barani Ulaya huku timu za Chelsea na Manchester City zikitazamia kubadilisha matokeo ya mkondo wa kwanza ili kujihakikishia nafasi ya kufuzu robo fainali. Saa tatu kasorobo itashuhudia Bodo Glimt wakisafiri kuelekea ureno kuchuana na Sporting Lisbon ambapo Glimt wanalenga kufuzu robo fainali haswa baada ya […]

KENYA YAANDAA MASHINDANO YA DAVIS CUP AFRIKA

Shirikisho la Tenisi nchini limepata haki ya kuandaa mashindano ya Davis Cup Africa Group IV yatakayofanyika mwezi Juni, hatua inayorejesha mashindano makubwa ya tenisi ya bara Afrika katika jiji la Nairobi. Mashindano hayo ya siku nne yatakutanisha mataifa manane ambayo ni Algeria, Angola, Botswana, Democratic Republic of the Congo, Ghana, Mozambique, Zimbabwe na Kenya, zikishindana […]

3K FC YAMTANGAZA OMASETE KUWA KOCHA MKUU

Klabu ya 3K FC inayoshiriki Ligi ya National Super League imemthibitisha Nicodemus Omasete kuwa kocha wake mkuu mpya baada ya kuonyesha kiwango bora alipokuwa kama kocha wa muda. Omasete anachukua nafasi ya Francis Chege kufuatia kushuka kwa matokeo kulikosababisha mabadiliko katika benchi la ufundi. Tangu achukue majukumu hayo, Omasete ameiongoza timu hiyo kushinda mechi sita mfululizo […]

WAJUMBE WA ODM NAIROBI WAMUIDHINISHA WINNIE ODINGA KAMA MWAKILISHI WA NAIROBI

Wajumbe wa ODM katika kaunti ya  Nairobi wamemuidhinisha Winnie Odinga kuwa mwakilishi wa eneo Bunge la Kibra na jimbo la Nairobi kiujumla , hatua ambayo maafisa wa chama wanasema itafungua njia yake kuingia katika Baraza la Kitaifa la Uongozi la chama hicho. Uamuzi huo umefikiwa wakati wa mkutano wa wajumbe wa ODM Nairobi uliofanyika katika ukumbi wa JOOF ukiongozwa na mwenyekiti wa chama […]

NATEMBEYA AONYA MADAKTARI WA UMMA WANAOPUUZA WAGONJWA

Gavana wa Kaunti ya Trans Nzoia George Natembeya amesema serikali yake haitavumilia madaktari walioajiriwa na umma wanaoshindwa kuwahudumia wagonjwa ipasavyo. Natembeya ameeleza kuwa baadhi ya madaktari wanatumia muda mwingi kuendesha kliniki zao binafsi badala ya kutekeleza majukumu yao katika hospitali za serikali, hali inayodhoofisha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi. Ameonya kuwa hatua kali […]