RUTO AAHIDI KUILINDA HOSPITALI YA NAIROBI DHIDI YA WAHUJUMU

Rais William Ruto amevunja ukimya wake kuhusu mzozo unaoikumba The Nairobi Hospital, akiahidi kuilinda dhidi ya watu aliowataja kuwa matapeli wanaotaka kuihujumu. Kwa mujibu wa Rais, baadhi ya maafisa wa hospitali hiyo walimfikia wakitaka aingilie kati kuhusu madai ya jaribio la kuiteka, ombi ambalo amesema atalishughulikia kwa dhati. Wakati huo huo, Ruto amesema ameagiza hatua za […]

MANYURU ATAKA USHIRIKIANO KUIMARISHA PVK

Mwenyekiti wa Pentecostal Voice of Kenya ambaye pia ni mchungaji wa Jesus Teaching Ministry, Apostle Peter Manyuru, amewataka wanachama wa muungano huo kushirikiana ili kuhakikisha ukuaji wa chama cha PVK. Manyuru amesema ushirikiano huo utachangia kuimarisha wanachama, kuleta umoja na kuchochea ukuaji wa chama pamoja na makanisa yaliyo chini ya muungano huo. Aidha, amewarai viongozi […]

NCPB YACHUKUA KAZI YA RUZUKU YA MBEGU KUTOKA KAMPUNI YA MBEGU

Bodi ya Kitaifa ya Nafaka na Mazao (NCPB) imeagizwa kuwajibika kwa mpango wa ruzuku ya mbegu ya mahindi kutoka kwa Kampuni ya Mbegu, kufuatia kikao cha Kamati ya Bunge ya Kilimo na Mifugo tarehe 16 mwezi huu. Hatua hiyo inalenga kurahisisha usambazaji wa mbegu za ruzuku katika msimu wa upanzi unaoendelea na kuhakikisha wakulima wanapata […]

MVUA KUBWA KUENDELEA KUNYESHA- UTABIRI

Idara ya utabiri wa hali ya anga imewataka wakenya kujiandaa kwa mvua kubwa kati ya leo na tarehe 23 mwezi huu, itakayonyesha katika maeneo kadhaa nchini. Kwenye taarifa yake ya kila wiki, idara hiyo imesema mvua hiyo huenda ikaongezeka Alhamisi wiki hii, ikitarajiwa katika maeneo kama vile nyanda za juu za mashariki na magharibi mwa […]

RUTO, MUSEVENI KUZINDUA SGR YA KISUMU-MALABA

Shughuli za kibiashara na uchukuzi zinatarajiwa kurahishwa kati ya Kenya na Uganda kutokana na uzinduzi wa ujenzi wa reli ya kisasa, SGR, kutoka Kisumu kuelekea Malaba. Kulingana na Waziri wa uchukuzi Davis Chirchir, uzinduzi huo utafanywa kwa pamoja na Rais William Ruto na mwenzake wa Uganda Yoweri Museveni. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

SHIRIKA LAPINGA UTEKELEZWAJI WA SHERIA YA HAZINA YA MIUNDOMBINU

Kesi imewasilishwa katika mahakama kuu ya Milimani kupinga utekelezwaji wa sheria ya hazina ya miundomsingi ya shilingi trilioni 5, kwa misingi kwamba sheria hiyo ya mwaka 2026 inakiuka katiba. Walalamishi ambao ni Katiba Institute, wanaitaka mahakama kutoa amri za kuzuia utekelezwaji wa sheria hiyo, pamoja na kuizuia serikali kutuma fedha za mauzo ya mashirika ya […]

MBAPPE KIKOSINI, BELLINGHAM NJE DHIDI YA CITY

Mshambulizi wa Real Madrid Kyllian Mbappe amejumuishwa kwenye kikosi cha klabu hiyo kitakachomenyana na Manchester City leo usiku kwenye mechi ya mkondo wa pili ya raundi ya 16 ya ligi ya klabu bingwa bara Ulaya. Mbappe mwenye umri wa miaka 27 ambaye alikosa mkondo wa kwanza kutokana na jeraha la goti, anatarajiwa kuongoza mashambulizi dhidi […]

ULINZI STARS WAWATIMUA MAKOCHA OCHOLLA, ONYISO

Klabu ya Ulinzi Stars imemsimamisha kazi kwa muda kocha mkuu Stephen Ocholla na msaidizi wake Francis Onyiso, kutokana na matokeo duni ambayo yameshuhudia klabu hiyo ikicheza mechi 9 bila ushindi. Matokeo hayo duni yamewaacha wanajeshi hao wakishikilia nafasi ya pili kutoka chini mwa jedwali, wakiwa na pointi 19 pekee baada ya mechi 24. Kichapo cha […]

WANNE WAFARIKI KWENYE JENGO SHAURI MOYO

Shughuli za uokoaji zinaendelea mtaani Shauri Moyo jijini Nairobi ambako jumba moja limeporomoka na kuwaua watu 4 huku wengine 4 wakiokolewa. Kwa mujibu wa wizara ya usalama wa kitaifa, jumba hilo ni miongoni mwa mijengo inayoendelea kubomolewa na tume inayosimamia uimarishaji wa Nairobi River katika eneo la Blue Estate, karibu na mto huo. Watu zaidi […]

WAKENYA WAKATALIWA NA JESHI LA URUSI

Serikali ya Kenya italazimika kutafuta njia mbadala ya kuwarejesha nchini wakenya waliotia saini mkataba kupigana kwenye vita kati ya Urusi na Ukraine, baada ya Urusi kudinda kugharamia usafiri huo kwa misingi kwamba hakuna makubaliano ya kugharamia usafiri huo kwenye kandarasi zao. Haya yamebainika baada ya mkutano wa faragha kati ya mkuu wa mawaziri Musalia Mudavadi […]