SAKAJA AAGIZA MPANGO WA SAA 48 KUKABILI MAFURIKO NAIROBI

Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja ameagiza kuandaliwa kwa mpango wa hatua za saa 48 ili kukabiliana na mafuriko, matatizo ya mifereji ya maji na uharibifu wa miundombinu katika jiji la Nairobi. Agizo hilo lilitolewa baada ya mkutano wa dharura uliofanyika katika City Hall uliowaleta pamoja maafisa wa serikali ya kaunti na mashirika ya serikali ya […]

RUTO ASUTA UPINZANI WAKATI WA ZIARA MAGHARIBI

Rais William Ruto amewashutumu viongozi wa upinzani akisema hawana ajenda madhubuti kwa Wakenya akidai kuwa hawajawasilisha mpango wowote unaolenga kuboresha maisha ya Wakenya.  Akizungumza wakati wa ziara yake katika eneo la Magharibi mwa nchi, Rais amesema baadhi ya wanasiasa wanajihusisha zaidi na siasa badala ya kutoa suluhu kwa changamoto zinazowakabili wananchi Ziara ya Rais katika eneo […]

MAAFISA WA NAIROBI HOSPITAL MAHAKAMANI

Maafisa kadhaa wa Nairobi Hospital wamefikishwa katika mahakama ya Milimani baada ya kukamatwa katika njia tatanishi kuhusiana na makosa ambayo hayajawekwa wazi. Maafisa hao ni mshauri wa matibabu ya wanawake Dakta Job Obwaka, naibu mwenyekiti wa bodi ya hospitali hiyo Samson Kinyanjui, mkurugenzi Valery Gaya na mkurugenzi wa zamani Chris Bichage. Kukamatwa kwao kumekosolewa na […]

KESI DHIDI YA MWALIMU ‘ALIYEMPA’ MWANAWE SUMU KUANZA APRILI

Mahakama kuu jijini Eldoret imepanga tarehe 21 mwezi ujao kuwa tarehe ya kusikiliza kesi ya mauaji inayomkabili mwalimu mmoja wa shule ya msingi, Sylivia Bosibori, anayekabiliwa na tuhuma za kumwua mwanawe mvulana mwenye umri wa miaka 9 kwa kumpa sumu miaka 5 iliyopita. Hakimu Emily Ominde ametoa agizo hilo baada ya upande wa mashtaka kuiarifu […]

BEI ZA PETROLI, DIZELI, NA MAFUTA TAA KUSALIA ZILIVYO – EPRA

Ni afueni kwa mwananchi baada ya mamlaka ya mafuta na udhibiti wa nishati nchini EPRA kutangaza kuwa Bei za mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa hazitaongezwa katika ukaguzi wa hivi punde kati ya Machi 15, 2026 hadi Aprili 15, 2026.Hii ina maana kwamba, jijini Nairobi, lita moja ya petroli itaendelea kuuzwa kwa Ksh.178.28, huku […]

WAKULIMA TRANS NZOIA WAPINGA RUZUKU YA MBEGU

Wakulima katika kaunti ya Trans Nzoia wametofautiana na mpango wa ruzuku kwa mbegu za mahindi uliotolewa na wizara ya kilimo wiki jana, wakisema bei zilizopunguzwa haziambatani na gharama ya uzalishaji wa mahindi. Kwa mujibu wa wakulima hao, wizara ya kilimo ilipaswa kuwashirikisha kupitia vikao vya kukusanya maoni ili kubaini bei hitajika ya mbegu hizo. Licha […]

ICHUNG’WA ATAKA SHULE ZIZUIWE KUUZA SARE

Wizara ya elimu imetakiwa kubuni sera itakayozuia shule kujihusisha na biashara za kuwauzia wanafunzi sare, ili kuwapa wazazi uhuru wa kununua sare hizo katika maduka wanayopendelea. Akizungumza katika eneo la Uriri, kiongozi wa wengi katika bunge la kitaifa Kimani Ichung’wa, amesema shule nyingi zimekuwa zikiwashinikiza wazazi kununua sare hizo kwa bei ya juu shuleni. Aidha, […]

RUTO AANZA ZIARA MAGHARIBI

Wakazi wa eneo la Magharibi mwa nchi wanatarajia kunufaika na uzinduzi wa miradi ya maendeleo utakaoongozwa na Rais William Ruto, ambaye ameanza ziara yake ya siku 4 katika kaunti zote 4 za eneo hilo. Katika kaunti ya Busia anakoanzia ziara hiyo, Rais atazindua ujenzi wa barabara za Mundere Okando-Sio Port-Nangina- Matayos-Namusira-Nasewa, na Matayos-Nangina-Sio-Port-Mubaka, na masoko […]

MATIANG’I AKOSOA MATUMIZI YA FEDHA IKULU

Mwaniaji wa urais kupitia chama cha Jubilee Fred matiang’i, ameahidi kupunguza matumizi ya fedha za Ikulu kwa asilimia 80 iwapo wakenya watamchagua kuwa Rais kwenye uchaguzi mkuu ujao. Akirejelea ripoti za mdhibiti wa bajeti ya serikali, Matiang’i amekosoa madai ya ubadhirifu wa fedha za umma katika Ikulu, akisema fedha zinazotengewa ikulu kwa sasa ni ukosefu […]

TUDOR AAMINI ALAMA DHIDI YA LIVERPOOL MWAMKO KWA SPURS

Kaimu kocha mkuu wa Tottenham Ingor Tudor, amepongeza juhudi za wachezaji wake zilizowapa pointi moja muhimu dhidi ya bingwa mtetezi wa EPL Liverpool, na kuwapa matumaini ya kukwepa shoka la kushushwa daraja. Bao la Richarlison katika dakika ya 90 liliwapa Spurs sare ya bao 1-1 ugani Anfield, na kutamatisha msururu wa kichapo katika mechi 6 […]