KENYA CUP: KABRAS RFC WAMALIZA KILELENI

Klabu ya Kabras RFC ilidhihirisha ubabe wao katika mchezo wa raga nchini kwa kuandikisha ushindi wa 27-13 dhidi ya Menengai Oilers ugani ASK Grounds mjini Kakamega, na kumaliza kileleni mwa msimu kawaida katika ligi ya Kenya Cup. Ushindi huo uliwafikishia pointi 52 kileleni kutokana na mechi 11, pointi 2 mbele ya KCB RFC. Timu hizo […]

GOR WAKANYAGA GWARIDE KUELEKEA UBINGWA

Viongozi wa ligi kuu ya soka nchini, KPL, Gor Mahia, waliendelea na msafara wao wa kuelekea ubingwa wa ligi hiyo msimu huu baada ya kuandikisha ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya wanajeshi wa Ulinzi Stars hapo jana. Green Commandos walivunja ngome ya Ulinzi ndani ya dakika 9 za kwanza, Enoch Morrison akifunga kupitia mkwaju wa […]

MZOZO WA UONGOZI KWENYE BODI YA NAIROBI HOSPITAL

Mkurugenzi wa chama cha madaktari nchini, KMA, Job Obwaka, ambaye pia ni mtaalamu wa afya ya wanawake katika Nairobi Hospital, na naibu mwenyekiti wa bodi ya hospitali hiyo Samson Kinyanjui, wanatarajiwa kufikishwa mahakamani hii leo baada ya kukamatwa wikendi kuhusiana na makosa yasiyofahamika. Wawili hao wamekesha katika kituo cha polisi cha Muthaiga, muungano wa madkatari […]

NDETI AWATAKA WAKAZI KUTAHADHARI MAPEMA

Huku mvua kubwa ikibashiriwa kuendelea nchini, wakazi wa kaunti ya Machakos wametakiwa kuwa makini na kuhamia maeneo yaliyo salama ili kuepusha majanga yanayoweza kusababishwa na mafuriko. Gavana wa kaunti hiyo Wavinya Ndeti, amesisitza haja ya wakazi kujihakikishia usalama kwa kuchukua tahadhari ya mapema. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

HASARA, MAAFA YA MAFURIKO

Idadi ya watu waliofariki kutokana na mafuriko nchini imethibitishwa kufikia 66 huku maelfu ya wengine wakiendelea kukadiria hasara, idara ya polisi ikisema zaidi ya watu 2,000 wamehamishwa na mafuriko kwa lazima. Jijini Nairobi, usimamizi wa mradi wa uimarishaji wa Nairobi River umeorodhesha sehemu 37 kama zilizo kwenye hatari ya kufurika, wakazi wakitakiwa kuchukua tahadhari wakati […]

TUJU AAPA KUPIGANI ARDHI ILIYONADIWA

Aliyekuwa katibu mkuu wa chama cha Jubilee Raphael Tuju, amesisitiza kuwa hatalegeza juhudi za kupigania kipande chake cha ardhi cha ekari 27 kilicho mtaani Karen jijini Nairobi, licha ya kupigwa mnada. Kwa mujibu wa mbunge huyo wa zamani, kiasi cha fedha anazodaiwa na benki moja ni kidogo mno ikilinganishwa na thamani ya ardhi hiyo. Ameibua […]

UPINZANI WADAI NJAMA YA UBADHIRIFU KUPITIA UBINAFSISHWAJI

Muungano wa upinzani nchini umeibua hofu kuhusu uwepo wa njama ya watu mashuhuri serikalini kunufaika na mpango wa ubinafsishaji wa mashirika ya umma, na kumtaka Rais William Ruto kuweka wazi mpango huo. Wakiongozwa na vinara Kalonzo Musyoka wa Wiper, Rigathi Gachagua wa DCP na Eugene Wamalwa wa DAP-K, viongozi hao wamedai kuwa Rais Ruto amekuwa […]

MAHAKAMA YAZUIA NYONGEZA YA ADA ZA ARDHI KAHAWA

Wakazi wa Kahawa Sukari kaunti ya Kiambu wamepata afueni ya muda baada ya mahakama kuu kutoa amri ya kuzuia serikali ya Kiambu dhidi ya kutekeleza nyongeza ya ada za ardhi hadi kesi itakaposikilizwa na kuamuliwa. Kwenye uamuzi wake, jaji Mogeni ameagiza kuwa amri ya muda itolewe ili kuzuia utekelezaji huo hadi mwafaka utakapotolewa. Kulingana na […]

WAKULIMA WA MAHINDI KUUZIWA MBEGU NAFUU

Wakulima wa mahindi nchini wanaojiandaa kwa upanzi msimu huu wamepata afueni kufuatia hatua ya serikali kuweka ruzuku kwa mbegu za mahindi, ikiwa ni sehemu ya serikali kuimarisha uzalishaji wa chakula cha kutosha. Kupitia taarifa, katibu mkuu katika wizara ya kilimo Kipronoh Ronoh, amefichua kuwa serikali imetenga shilingi bilioni 2 kufanikisha ruzuku hiyo, itakayopelekea kupungua kwa […]

UNAI EMERY AWEKA REKODI KWENYE USHINDI WA VILLA

Kocha mkuu wa Aston Villa Unai Emery amekuwa kocha wa tatu kufikisha ushindi 100 kwa kasi kati ya makocha 3, kikosi chake kilipoandikisha ushindi wa bao 1-0 ugenini dhidi ya Lille ya Ufaransa jana usiku. Ushindi huo umewapa Villa usukani wa kujiendesha kueleka awamu ya robo fainali ya ligi ya UEFA UROPA msimu huu. Mhispania […]