JUNIOR STARLETS YATAJA KIKOSI CHA AWALI
Kocha wa Junior Starlets Mildred Cheche ametaja kikosi cha awali cha wachezaji 30 kuelekea mechi za kufuzu Kombe la Dunia kwa wasichana chini ya miaka 17 dhidi ya Uganda.
Cheche amedumisha sehemu kubwa ya kikosi kilichofanya vyema katika raundi iliyopita ambapo waliifunga Namibia kwa jumla ya mabao 7–1 na kufuzu hatua inayofuata.
Kikosi hicho kinatarajiwa kuripoti kambini tarehe 6 Mei katika uwanja wa Kasarani Annex, ambapo wachezaji 23 wa mwisho watachaguliwa kabla ya mechi hiyo muhimu.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 














































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































