#Local News

CHERARGEI AWASILISHA HOJA YA KUSITISHA MARUPURUPU YA UHURU

Seneta wa Nandi Samson Cherargei amewasilisha hoja katika Seneti akitaka kusitishwa au kupunguzwa kwa marupurupu ya Rais mstaafu Uhuru Kenyatta.

Kupitia hoja hiyo, Cherargei anataka Bunge kufuta, kubadili au kugawa upya fedha zinazohusiana na marupurupu ya kiongozi huyo wa zamani, akipendekeza fedha zitakazookolewa zielekezwe kwa maslahi ya wananchi.

Hatua hiyo inajiri wakati washirika wa Rais William Ruto wakiendelea kumkosoa Uhuru kutokana na msimamo wake wa kisiasa.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *