KENYA YALIPA ADA YA AFCON

Baada ya wiki kadhaa za kutokuwa na uhakika, Kenya imelipa ada ya kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) yenye thamani ya dola milioni 30 (Sh3.9 bilioni), Waziri wa Michezo, Salim Mvurya, amesema kuwa nchi imetekeleza mahitaji yote yaliyowekwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF). Aidha ameongeza kuwa serikali imepanga upya Kamati ya Kuandaa Mashindano (LOC) […]

GACHAGUA AKOSOA UBOMOAJI GIKOMBA

Aliyekuwa Naibu Rais, Rigathi Gachagua, amelaani ubomoaji uliofanyika usiku katika soko la Gikomba, akiutaja kuwa usio na utu, wa kikatili na unaolenga kuwadhulumu wafanyabiashara wadogo. Akizungumza na wanahabari Jumanne, Machi 31, 2026, huko Makueni, Gachagua aliishutumu serikali kwa kupanga ubomoaji huo usiku, akisema hatua hiyo ni mateso kwa wananchi wanaojitafutia riziki. Alidai kuwa maelfu ya […]

SERIKALI YATOA HAKIKISHO LA MAFUTA

Waziri wa Nishati na Petroli, Opiyo Wandayi, amewahakikishia Wakenya kuwa nchi ina akiba ya kutosha ya mafuta licha ya mataifa kadhaa barani Afrika kukumbwa na uhaba. Akizungumza kufuatia taarifa za foleni ndefu katika vituo vya mafuta katika baadhi ya nchi, Wandayi amesema Kenya haijakumbwa na upungufu wowote na inaendelea kuwa na usambazaji thabiti wa bidhaa […]

GAVANA WATAKA HATI ZA KUKAMATWA ZIONDOLEWE

Baraza la Magavana limetaka kuondolewa mara moja kwa hati zozote za kukamatwa na hatua za shinikizo dhidi ya magavana, kukisubiriwa suluhu ya mzozo unaoendelea na Kamati ya Seneti ya Hesabu za Kaunti. Akizungumza na wanahabari Mwenyekiti wa baraza hilo, Ahmed Abdullahi, amesema hatua hiyo inalenga kulinda utaratibu wa kisheria na kuzuia kile alichokitaja kuwa kuingizwa kwa siasa […]

SENETI YAIDHINISHA MGAWANYO WA MAPATO

Kamati ya Kudumu ya Seneti kuhusu Fedha na Bajeti imeidhinisha ripoti yake kuhusu Mswada wa Mgawanyo wa Mapato kwa mwaka wa fedha wa 2026/2027, hatua inayofungua njia kwa mjadala bungeni. Kwa mujibu wa taarifa ya Bunge iliyochapishwa hii leo, maseneta wamejadili athari za upungufu wa mapato ya kitaifa kwa serikali za kaunti. Kamati hiyo imebainisha kuwa ukusanyaji mdogo […]

KINDIKI AWATAKA MABALOZI KUITANGAZA KENYA

Naibu Rais, Kithure Kindiki, amewataka mabalozi wa Kenya kuitangaza nchi kama salama na yenye fursa za uwekezaji, akisema ni jukumu lao kuvutia wawekezaji na wageni. Akizungumza wakati wa kufunga kongamano la 19 la mabalozi jijini Nairobi, Kindiki amesisitiza umuhimu wa mabalozi kushiriki kikamilifu katika kukuza taswira ya taifa kimataifa. Aidha ameongeza kuwa Kenya imepiga hatua kubwa […]

SILVA ATANGAZA KUONDOKA MAN CITY

Nahodha wa klabu ya Manchester City Bernardo Silva, amearipotiwa kuiarifu klabu hiyo kuhusu kuondoka kwake mwishoni kwa msimu huu. Kandarasi ya kiungo huyo raia wa Ureno mwenye umri wa miaka 31, itakamilika mwezi Juni mwaka huu, na ameonyesha ari ya kujiunga na klabu kadhaa bila ada yoyote. Silva alijiunga na City mwaka wa 2017, na […]

MKUFUNZI WA TUSKER AKIRI HANA UWEZO KUIPIKU GOR KPL

Kocha mkuu wa klabu ya Tusker Julien Mette, amekiri kwamba timu hiyo haitashinda taji la ligi kuu ya kandanda nchini, KPL, msimu huu, akisema hamna nafasi za kuipiku viongozi Gor Mahia. Tusker mara ya mwisho walishinda taji hilo mwaka wa 2016, na licha ya kutarajiwa kutamatisha kiu cha mwongo mmoja, Mette amesema lengo lao msimu […]

STARS WAILAZA GRENADA KUMALIZA WA TATU FIFA SERIES

Timu ya taifa ya kandanda ya wanaume Harambee Stars ilitamatisha kinyang’anyiro chao cha FIFA Series nchini Rwanda kwa ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Grenada kutoka bara Ulaya, kwenye mechi iliyosakatwa katika uwanja wa Amahoro jijini Kigali. Kutokana na ushindi, Kenya ilimaliza ya tatu, nyuma ya Estonia waliolazwa mabao 2-0 na mabingwa Rwanda kwenye […]

WAATHIRIWA WA MAANDAMANO WATAKA MUDA ZAIDI

Huku zikiwa zimesalia siku 2 kabla ya kukamilika kwa muda waliopewa waathiriwa wa maandamano kuwasilisha stakabadhi hitajika ili kuzingatiwa kwa fidia, familia za waathiriwa hao zimeitaka tume ya kitaifa kuhusu haki za kibinadamu kuziongeza muda zaidi. Miongoni mwa malalamishi ya familia hizo ni ukosefu wa mawasiliano ya kutosha pamoja na njia mwafaka za kuifikia tume […]