UHABA WA MAFUTA WANUKIA

Serikali imejiandaa kuwalinda wakenya dhidi ya bei ghali ya mafuta kutokana na uhaba wa bidhaa hiyo unaotarajiwa kufikia katikati mwa mwezi huu, ikisema itatumia takribani shilingi bilioni 17 kutoka hazina ya udhibiti wa bei kuwakinga wakenya dhidi ya bei ya juu ila kwa kipindi kifupi. Akiwa mbele ya kamati ya bunge la kitaifa kuhusu fedha […]

UPINZANI, SERIKALI WAVUTANA KUHUSU UBOMOAJI GIKOMBA

Vuta nikuvute baina ya serikali na muungano wa upinzani imeendelea kuhusu mpangilio mpya wa soko la Gikomba jijini Nairobi, muungano wa upinzani sasa ukiwataka wafanyabiashara sokoni humo kupinga kuhamishwa. Wakiongozwa na kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka, viongozi wa upinzani wamedai kuna njama ya kunyakua ardhi ya soko hilo kwa kuwahamisha wafanyabiashara, huku serikali ikisema inawahamisha […]

UJUMBE WA RUTO KUHUSU PASAKA

Huku Wakristo kote ulimwenguni wakiadhimisha siku kuu ya Pasaka, Rais William Ruto amewatakia Pasaka njema huku akiwahimiza kuitumia kutafakari kuhusu mwanzo mpya maishani mwao. Kupitia kanda fupi ya video aliyoichapisha kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii, Ruto amesema kipindi cha Pasaka ni mwanzo mpya miongoni mwa familia za wakenya na kuwataka kuliombea taifa. Amewataka […]

NTSA YATAKA KESI YA FAINI KUTUPILIWA MBALI

Mamlaka ya Kitaifa ya Usalama Barabarani, NTSA, imeiomba Mahakama Kuu kutupilia mbali kesi inayopinga utekelezaji wa mfumo wa faini za papo hapo, ikisema suala hilo limepitwa na wakati. Katika hati ya kujibu, mkurugenzi mkuu wa NTSA, Odhiambo Kondiwa, amesema mamlaka hiyo ilisitisha rasmi mpango huo Machi 27 mwaka huu hivyo kesi hiyo haina msingi wa kuendelea kusikilizwa. Kesi […]

MOTO WATEKETEZA NYUMBA ZA MAGEREZA LANG’ATA

Idara ya magereza nchini imethibitisha kuwa moto umeteketeza nyumba 30 za makazi ya maafisa katika Gereza la Wanawake la Lang’ata lenye ulinzi mkali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na idara hiyo moto huo ulizuka Jumatano jioni majira ya saa moja na nusu na kuteketeza nyumba hizo kabisa. Hata hivyo, idara hiyo imesema hakuna mtu aliyepoteza maisha au kujeruhiwa, huku […]

SERIKALI KUTOA VITAMBULISHO KUANZIA SHULE YA UPILI

Katibu wa Idara ya Uhamiaji na Huduma za Wananchi, Belio Kipsang, ameongoza zoezi la kuwahamasisha machifu kuhusu mwongozo mpya wa kuwasajili Wakenya waliofikisha miaka 18 kupata vitambulisho vya kitaifa. Zoezi hilo lililoanza mwezi Julai mwaka jana katika kaunti 20 limewezesha usajili wa watu milioni 1.7 hadi sasa, huku Kipsang akisema waombaji watapata vitambulisho ndani ya […]

WAKENYA 16 WARIPOTIWA KUPOTEA URUSI

Waziri Mkuu wa Mawaziri na Waziri wa Mambo ya Nje, Musalia Mudavadi, amesema angalau Wakenya 16 wameripotiwa kupotea nchini Urusi. Mudavadi amesema idadi hiyo imeongezeka kutoka watu 10 hadi 16 ndani ya saa 24 zilizopita, huku hali halisi ya walipo bado haijabainika. Ameeleza kuwa suala hilo limezua wasiwasi mkubwa kitaifa, hasa kutokana na madai ya […]

MBADI: BEI YA MAFUTA IMEPANDA KIMATAIFA

Waziri wa Hazina ya Taifa, John Mbadi, amesema serikali itaingilia kati kuwalinda Wakenya dhidi ya kupanda kwa bei ya mafuta ya petroli katika soko la kimataifa. Mbadi amesema serikali itatumia fedha kutoka kodi ya maendeleo ya mafuta, inayokadiriwa kuwa shilingi bilioni 17, katika kipindi cha miezi mitatu ijayo ili kupunguza shinikizo la bei kwa watumiaji. […]

BUNGOMA HIGH YALENGA UBINGWA WA RAGA

Timu ya raga ya Bungoma High School inalenga kurejea historia ya mwaka 2016 kwa kutwaa ubingwa wa kitaifa wa raga ya wachezaji 15 katika michezo ya shule za upili itakayofanyika Kisumu Hii ni baada ya ushindi wao wa kanda ya magharibi walipowashinda Kakamega School alama 12-07 katika fainali iliyofanyika Chavakali High School mwezi uliopita. Kocha wao, Titus […]

TUCHEL: FODEN HANA UHAKIKA NA NAFASI YA KOMBE LA DUNIA

Kocha wa uingereza, Thomas Tuchel, amesema nafasi ya Phil Foden katika kikosi cha Kombe la Dunia haijahakikishwa, baada ya mchezaji huyo kushindwa kuonyesha kiwango cha juu tena katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Japan. Foden, mwenye umri wa miaka 25, alikumbana na changamoto kucheza katika nafasi isiyo ya kawaida mbele, huku Harry Kane akikosa kwenye mchezo huo. […]