FIFA WORLD CUP: DR CONGO WAIZIMA JAMAICA, ITALIA NJE GYOKERES AKIBEBA SWEDEN

Timu ya taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC, ilijikatia tiketi ya kufuzu mashindano ya kombe la dunia kwa mara ya kwanza tangu miaka 52 iliyopita, baada ya kuilaza Jamaica bao 1-0 katika fainali ya mechi za mchujo wa mabara, Intercontinental play-off. Katika mechi iliyosakatwa katika uwanja wa Guadalajara nchini Mexico, kiungo wa Burnley […]

NAIBOIS, MARA SUGAR KUVAANA KPL

Ligi kuu ya soka ncini KPL inarajelewa hii leo ambako Nairobi United watamenyana na Mara Sugar katika uwanja wa Ulinzi Sports Complex, katika vita vya katikati mwa jedwali la ligi. Naibois walio katika nafasi ya 10 wakiwa na pointi 34 baada ya mechi 24, wamekuwa na msimu vuguvugu, wakiandikisha matokeo mseto. Mechi yao ya mwisho […]

SHUJAA WATUZWA NA ‘KUNDI GUMU’ UBINGWA HONG KONG 7S

Timu ya taifa ya raga ya wachezaji 7 kila upande, Shujaa, watakabiliwa na mtihani mgumu wa msimu wao baada ya kuwekwa kwenye Pool C inayoaminika kuwa ngumu katika mashindano ya 2026 HSBC SVNS World Championship yatakayosakatwa tarehe 17-19 mwezi huu jijini Hong Kong. Mashindano hayo yaliyo na timu 12 zilizogawanywa kwenye makundi 3, yatazikutanisha timu […]

UPINZANI WALALAMIKIA UHABA WA KIEMS

Tume huru ya uchaguzi na mipaka, IEBC, imetakiwa kutuma vifaa vya kutosha vya kielektroniki vya kuwasajili wapiga kura, mbali na maafisa wa kutosha ili kuhakikisha kila anayehitaji kusajiliwa anafikiwa. Ni wito uliotolewa na viongozi wa muungano wa upinzani wanaoendeleza ziara yao katika eneo la Ukambani, wakiibua madai ya uhaba wa vifaa hivyo katika mengi ya […]

UNAWEZA KUSAJILIWA KOKOTE, IEBC

Wakenya wanaolenga kusajiliwa kama wapiga kura wapya wana fursa ya kufanya hivyo katika eneo lolote waliko, na kuchagua kituo wanachopendelea kupiga kura. Hii ni kulingana na tume huru ya uchaguzi na mipaka, IEBC, ambayo imeendelea kuwahimiza wakenya kujitokeza huku ikilenga kuwasajili wapiga kura wapya milioni 2.5 ndani ya muda wa siku 30. Zoezi hilo linaendeshwa […]

PASAKA: POLISI WAIMARISHA DORIA

Idara ya polisi nchini imetangaza kuimarisha doria na utekelezaji kikamilifu wa sheria za trafiki ili kuimarisha usalama kuelekea siku kuu ya Pasaka inayoanza Ijumaa hii. Kupitia taarifa, inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja, amesema hatua hiyo ni kutokana na safari nyingi, mikusanyiko pamoja na mvua kubwa ambayo huenda ikaendelea kuneysha wakati wa siku kuu hiyo. […]

DCI YAFICHUA UOZO KATIKA KABURI LA PAMOJA KERICHO

Miili yote 33 iliyofukuliwa kutoka kaburi la pamoja katika eneo la Makaburini kaunti ya Kericho, ilitolewa katika makafani ya hospitali ya rufaa na mafunzo ya kaunti ya Nyamira, tofauti za taarifa za awali kwamba makafani hiyo iliruhusu miili 13 pekee. Kulingana na mkurugenzi wa idara ya upelelezi wa jinai, DCI, Mohammed Amin, uchunguzi wa awali […]

MASENETA WAKARIRI HAJA YA MAGAVANA KUAGIZWA

Huku mvutano ukiendelea kati ya maseneta na magavana kuhusu uwajibikaji wa matumizi ya fedha za umma, maseneta wamesisitiza umuhimu wa magavana kufika mbele ya bunge hilo kuweka wazi jinsi serikali zao9 zinavyowajibika mahitaji ya umma. Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna, amekariri kuwa kuna maswali mengi kuhusu matumizi ya fedha za umma katika kaunti mbali mbali […]

DE LA FUENTE AKARIBISHA TETESI ZA KUSHINDA KOMBE LA DUNIA

Kocha wa timu ya taifa ya Hispania, Luis de la Fuente, amesema anafurahia shinikizo la kuwa miongoni mwa wagombea wakuu wa kushinda Kombe la Dunia, akizungumza kabla ya mechi ya kirafiki dhidi ya Misri jijini Barcelona. De la Fuente amempongeza nyota, Lamine Yamal, huku akiepuka kusema iwapo ataanza mechi dhidi ya timu ya Misri, ambayo […]

BONDIA OYOKO AFARIKI ULINGONI

Sekta ya ndondi nchini inaomboleza kufuatia kifo cha bondia Jacob Oyoko maarufu kama “Jack Spoiler”, aliyedondoka wakati wa pambano la kulipwa katika Ukumbi wa Utamaduni wa Mumias, Kaunti ya Kakamega. Kifo hicho kilithibitishwa na rais wa Tume ya Ndondi za Kulipwa nchini, Reuben Ndolo, aliyesema bondia huyo wa Kisumu alifariki licha ya kupatiwa huduma ya […]