DHAHABU YA IKOLOMANI ITAWAFAIDI WAKAZI, BUNGE LAAHIDI
Bunge la kaunti ya Kakamega limewahakikishia wakazi wa eneo la Ikolomani kwamba litalinda maslahi yao wakati wa uchimbaji wa madini ya dhahabu ambao umeratibiwa kuanza hivi karibuni na mwekezaji wa kibinafsi.
Spika wa bunge hilo James Namatsi, amekiri kuwa bunge hilo limepokea malalamishi ya wakazi walio na hofu ya kudhulimiwa wakati wa zoezi hilo ambalo limezingirwa na utata.
Ameahidi vikao na usimamizi wa kampuni itakayochimba dhahabu hiyo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 














































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































