#Local News

AFISA WA ZAMANI WA KMPDC AKAMATWA KISA SHA

Maafisa wa DCI wamemkamata aliyekuwa mfanyakazi wa KMPDC, Harun Liluma, kuhusiana na tuhuma za ulaghai unaoathiri Social Health Authority (SHA).

Liluma anakabiliwa na mashtaka ya kula njama ya kutapeli, matumizi mabaya ya ofisi, kuingia bila idhini kwenye mifumo ya kompyuta na ulaghai wa kimtandao.

Waendesha mashtaka wanadai kuwa Liluma alitumia nafasi yake KMPDC kuwezesha usajili usio halali na malipo kwa vituo kadhaa vya afya, hatua iliyowaruhusu kudai fedha kutoka SHA kwa misingi ya uongo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *