SERIKALI YAHOFIA MAGENGE YA UHALIFU

Serikali imeibua hofu kuhusiana na kuchipuka kwa magenge ya uhalifu katika maeneo mbali mbali nchini, ikisema yamesababisha ongezeko la tishio la kiusalama. Akizungumza mbele ya bunge, Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen, amewashutumu baadhi ya viongozi wa kisiasa kwa madai ya kupanga na kufadhili magenge hayo ili kuvuruga hafla za kisiasa za wapinzani wao. […]

WANAFUNZI HEWA WAIFYONZA WIZARA MAMILIONI

Imefichuka kwamba serikali imekuwa ikipoteza shilingi milioni 91 kila mwaka kupitia wanafunzi hewa wapatao 900,000 katika shule za umma, huku shule hewa 27 pia zikitumiwa kufuja fedha za serikali licha ya kufungwa kutokana na sababu mbali mbali. Haya ni kulingana na ripoti ya ukaguzi wa wanafunzi katika shule za msingi na upili nchini ulioendeshwa na […]

ODM: MPASUKO WETU UNATOKA NJE YA CHAMA

Viongozi wa chama cha ODM sasa wamehusisha masaibu ya chama hicho na shinikizo kutoka nje ya chama, mrengo wa kinara Oburu Oginga ukimshutumu Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta kwa madai ya kuzua mgogoro huo kwa lengo la kuzuia mazungumzo ya ushirikiano wa kisiasa kati ya ODM na UDA kabla ya uchaguzi mkuu ujao. Kulingana na mrengo […]

HOFU YA USALAMA WA RAIS RUTO

Hofu imeibuka kuhusiana na usalama wa Rais William Ruto hasa kutokana na majaribio ya raia kumrukia akiwa majukwaani, tukio la hivi punde likiwa hapo jana ambapo Rais Ruto aliokolewa na walinzi kwenye jukwaa dhidi ya kukabiliwa na jamaa mmoja katika kaunti ya Wajir. Hatua hiyo ilimlazimu Rais kusitisha hotuba yake na kuangazia tukio hilo, ambalo […]

 RATCLIFFE: MAAMUZI MAGUMU MAN UNITED YAZAA MATUNDA

Mmiliki mwenza wa Manchester United, Jim Ratcliffe, amesema maamuzi magumu aliyoyachukua ambayo yamemfanya kuwa “asiye maarufu” miongoni mwa baadhi ya mashabiki sasa yanaanza kuzaa matunda. Ratcliffe amefanya mabadiliko kadhaa yenye utata tangu aliponunua hisa katika klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Uingereza miaka miwili iliyopita, ikiwemo kupunguza idadi ya wafanyakazi katika uwanja wa Old Trafford. […]

MOMANYI: TUSKER BADO WANA NAFASI YA UBINGWA

Nahodha wa Tusker FC Charles Momanyi amesisitiza kuwa mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya FKF bado ziko wazi kwa yeyote, akiamini kuwa Brewers wana uwezo wa kufanya mabadiliko makubwa na kuvuruga hesabu za wanaoongoza msimamo. Licha ya Tusker kushika nafasi ya nane kwa pointi 28, wakiwa nyuma kwa pointi 12 dhidi ya vinara Gor […]

Ideal Mobile Online Gambling Enterprises: A Full Guide

With the ever-increasing popularity of on-line casinos, it’s not a surprise that mobile gambling has actually become the following big thing in the sector. Gone are the days when gamers were constrained to their desktops; currently, they can enjoy their favored casino games on the go, anytime and anywhere. In this post, we’ll discover the […]

WASWA AAPA KUIPA AFC LEOPARDS UBINGWA

Mshambuliaji mpya wa AFC Leopards Andrew Waswa amesema analenga kuisaidia klabu hiyo kutwaa mataji msimu huu, akiahidi kutumia tajriba na mafunzo aliyopata nchini Uingereza kuimarisha kikosi cha Ingwe kwenye Ligi Kuu ya Kenya. Akizungumza baada ya kujiunga na klabu hiyo, Waswa amesema mafunzo yake katika chuo cha International House of Manchester yalimpa uzoefu wa kiwango […]

RISING STARLETS YAPANIA HATUA NYINGINE DHIDI YA TANZANIA

Rising Starlets wana matumaini ya kufuzu raundi inayofuata ya kufuzu Kombe la Dunia la FIFA kwa Wanawake chini ya miaka 20 wanapojiandaa kuvaana na Tanzania katika mechi ya marudiano itakayochezwa Jumamosi jijini Dar es Salaam. Kenya inaongoza kwa bao 1-0 kutoka mkondo wa kwanza uliochezwa Februari 7jijini Nairobi. Bao hilo la ushindi lilifungwa dakika za […]

SIFUNA APATA AFUENI YA MAHAKAMA

Katibu Mkuu wa chama cha ODM, Edwin Sifuna, amepata ushindi baada ya Mahakama ya Migogoro ya Vyama vya Kisiasa kusimamisha juhudi za kumfuta wadhifa wake. Mahakama hiyo imezuia utekelezaji wa azimio lililopitishwa na Kamati Kuu ya Kitaifa (NEC) ya ODM, linalolenga kumfukuza Sifuna. Aidha, mahakama imezuia wahusika kutangaza azimio hilo katika Gazeti la Kenya, hatua ambayo […]