KESI YA MAUAJI DHIDI YA AFISA WA POLISI KUENDELEA

Kesi ya mauaji inayomkabili afisa wa polisi Ahmed Rashid anayetuhumiwa kwa makosa ya kuwaua vijana wawili Jamal Mohammed na Mohammed Dhair Kheri Machi mwaka 2017 inatarajiwa kuendelea leo katika mahakama ya Kibra mbele ya hakimu Diana Kavedza. Mashahidi watatu akiwemo afisa kutoka idara ya upelelezi, DCI, na afisa wa mamlaka ya mawasiliano, CAK, wameratibiwa kutoa ushahidi wao katika kikao […]

SHOKA LA ODM LAWAANGUKIA WAASI BUNGENI

Wabunge wanaokosoa serikali jumuishi akiwemo Caroli Omondi, Anthony Kibagendi na mwakilishi wa kike wa kaunti ya Kisumu Ruth Odinga ni miongoni mwa waliofurushwa kutoka nyadhifa za uongozi wa bunge kutokana na msimamo wao, bunge likitishia kuwafurusha wakosoaji zaidi. Omondi ambaye amekuwa akihudumu kama mwenyekiti wa kamati ya utekelezaji wa katiba bungeni, amefurushwa na wadhifa wake […]

IEBC YATAKA BILIONI 1 KWA MAAKULI

Wabunge wametofautiana na bajeti ya shilingi bilioni 63.9 ya tume huru ya uchaguzi na mipaka, IEBC kufanikisha uchaguzi mkuu wa mwaka ujao, ambapo shilingi bilioni 1 zimetengewa chakula cha maafisa wa tume hiyo katika kipindi cha uchaguzi. Wakifika mbele ya kamati ya haki na masula ya kisheria bungeni, maafisa wa IEBC wamesema kwamba wanahitaji shilingi […]

WANDAYI ATETEA KUJIHUSISHA NA SERIKALI

Waziri wa kawi Opiyo Wandayi, ametetea kujihusisha kwake na shughuli za kisiasa nchini licha ya ukosoaji kutokana na wadhifa wake serikalini, akisema amekuwa akitumia majukwaa hayo kuwaeleza wakenya kuhusu utendakazi wa serikali. Akizungumza kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga, Wandayi amepuzilia mbali kwamba hatua hiyo ni sawa na kampeni za mapema za kumpigia debe […]

WANYAKUZI WAFIKIA ARDHI YA IKULU

Suala la unyakuzi wa ardhi ya umma limeonekana kuvuka mipaka, ikiibuka kwamba ardhi ya Ikulu ndogo katika kaunti za Kisumu, Uasin Gishu na Nakuru zimenyakuliwa na watu binafsi. Kwa mujibu wa msimamizi wa Ikulu Katoo Ole Metito akizungumza mbele ya kamati ya bunge kuhusu usalama, mwakilishi wadi mteule amejenga makazi yake kwenye ardhi ya Ilulu […]

UCL: INTER MILAN KUTAFUTA USHINDI DHIDI YA BODO GLIMT

Ligi kuu ya mabingwa barani ulaya hatua ya mwondoano itarejelewa hii leo kwa mkondo wa pili huku mechi kadhaa zikiratibiwa kuchezwa, Inter Milan watakua nyumbani San Siro wakitafuta kubatilisha matokeo ya wiki iliyopita walipochapwa mabao 3-1 na Bodo Glimt. Inter lazima washinde mchezo wa leo ili kufuzu hatua nyingine. Mechi nyingine zitakazochezwa ni pamoja na […]

BARCELONA YAMSAJILI CHIPUKIZI AJAY TAVARES

Klabu ya FC Barcelona imemsajili mchezaji chipukizi Ajay Tavares kutoka akademi ya Norwich City. Tavares, mwenye umri wa miaka 16, anaripotiwa kuvutia vilabu kadhaa barani Ulaya. Norwich itapokea fidia ya malezi, ingawa haijathibitisha kiasi cha fedha kinachohusika katika makubaliano hayo. Mchezaji huyo alijiunga na Norwich akiwa chini ya umri wa miaka 12. Msimu uliopita alitokea […]

KATASI ANG’ARA LIGI KUU YA KPL

Kipa wa AFC Leopards, Humphrey Katasi, ameendelea kuwa tegemeo muhimu kwa timu hiyo katika msimu uliogubikwa na ushindani mkali. Akiwa na mechi 10 bila kuruhusu bao, Katasi anaongoza orodha ya makipa wenye mechi nyingi safi katika SportPesa Premier League na yuko katika nafasi nzuri ya kuwania tuzo ya kipa bora wa msimu. Katasi anaongoza kwa […]

KOCHA WA LUANDA VILLA AAMINI TIMU ITANUSURIKA NSL

Kocha mkuu wa Luanda Villa, Francis Chinjili, amesema ana imani kuwa timu yake itaendelea kusalia katika Ligi ya Daraja la Kwanza, maarufu kama National Super League. Chinjili amepuuza madai kuwa yuko chini ya shinikizo la kubadilisha hali ya timu hiyo ambayo imekuwa ikikumbwa na mabadiliko ya mara kwa mara ya makocha. Tangu achukue usukani Januari […]

VIONGOZI WA KENYA KWANZA KIPSIGIS WAMKOSOA GACHAGUA

Viongozi wa muungano wa Kenya Kwanza kutoka jamii ya Kipsigis wamemkashifu aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua kwa matamshi yake kuwa jamii ya Kalenjin haina kiongozi anayezungumza kwa niaba yake. Viongozi hao wakiongozwa na Kiongozi wa Wengi katika bunge Seneti, Aaron Cheruiyot, wamesema kauli za Gachagua hazina msingi na zinalenga kuleta ubabe wa kisiasa ndani ya jamii hiyo. […]