BEATRICE CHEBET NJE YA UWANJA 2026

Mshindi wa nishani ya dhahabu 2 katika mbio za mita 10,000 na mita 5,000 katika mashindano ya Paris Olympics 2024 Beatrice Chebet atakuwa nje ya mashindano mwaka huu baada ya kuchukua likizo ya kujifungua. Haya ni kulingana na tangazo la ajenti wake, likimaanisha kwamba mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 25 hatatetea taji lake katika […]

MADURO ASISITIZA ANGALI RAIS WA VENEZUELA

Rais wa Venezuela aliyebanduliwa mamlakani na jeshi la Marekani Nicolas Maduro, amekana mashtaka ya ulanguzi wa dawa za kulevya na mashtaka mengine alipofikishwa katika mahakama za New York. Maduro mwenye umri wa miaka 63, amesisitiza kwamba angali rais wa Venezuela licha ya kubanduliwa na kutekwa nyara Jumamosi iliyopita.  Mkewe rais huyo Cilia Flores, pia amekana […]

AMOLLO: HATUJAPANGA KUMTIMUA SIFUNA

Naibu mwenyekiti wa chama cha ODM Otiende Amollo ambaye pia ni mbunge wa Rarieda, amesisitiza kuwa hakuna mchakato wowote ulioanzishwa wa kumtimua katibu mkuu wa chama hicho Edwin Sifuna jinsi inavyodaiwa. Kauli ya Amollo inajiri baada ya kuibuka mgawanyiko baina ya Sifuna na kiongozi wa walio wachache bungeni Junet Mohammed, kuhusu mchango wa shilingi milioni […]

HOFU YA AJALI BARABARANI

Hofu imeibuka nchini kuhusu ajali za barabarani, zaidi ya watu 20 wakiaga dunia kwenye ajali hizo katika kipindi cha siku 5 za mwanzo wa mwaka huu pekee huku wito ukitolewa kwa madereva kuwa makini. Hii ni baada ya watu 9 kufariki kwenye ajali katika eneo la Naivasha hapo jana na wengine 55 kujeruhiwa, ajali ambayo […]

UCHUNGUZI WA DCI KUHUSU KIFO CHA JIRONGO

Aliyekuwa mbunge wa Lugari Cyrus Jirongo alifariki kwenye ajali ya kawaida na wala hakuna uhalifu uliohusika kutokana na ushahidi uliopo. Haya ni kulingana na taarifa ya idara ya upelelezi DCI, ambayo imeripoti kuwahoji na kuandikisha taarifa kutoka kwa watu kadhaa akiwemo spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang’ula, dereva wa basi la Climax Coaches Tiras […]

WAZAZI NJIA PANDA KUHUSU GRADE 10

Baadhi ya wazazi wamejipata katika hali ya mkanganyiko kuhusu hatma ya masomo ya wanao wanaofaa kujiunga na gredi ya 10 wiki ijayo, baada ya kukumbwa na dosari katika mchakato wa kuwaweka katika shule za kujiunga nazo. Wakizungumza na wanahabari, wazazi waliokosa kurudhishwa na shule walizowekwa wanao wamelalamikia madai ya serikali kutojali, wakiitaka kuangazia upya mchakato […]

ALAI AKANA KUMSHAMBULIA BABU

Mwakilishi wa wadi ya Kileleshwa jijini Nairobi Robert Alai, amekana madai ya kumshambulia mbunge wa Embakasi East Babu Owino mtaani Kilimani. Kwenye mazungumzo na kituo kimoja cha runinga mapema leo, Alai amekiri kuwepo kwa majibizano baina yao kuhusu wadhifa wa ugavana kwenye uchaguzi mkuu ujao ila akakana kumshambulia. Wawili hao wanachunguzwa na polisi kuhusu madai […]

LUSAKA AHIMIZA UADILIFU SERIKALINI MWAKE

Maafisa wa serikali ya kaunti ya Bungoma wametakiwa kudumisha uadilifu, umoja na uwajibikaji serikali hiyo inapoangazia kuimarisha utendakazi na ukamilishaji wa miradi ya maendeleo iliyokwama. Akizungumza mapema leo kwenye kikao na wafanyakazi hao, gavana wa Bungoma Ken Lusaka amesema hatua hiyo ni muhimu katika utendakazi wa serikali hiyo kwa wananchi. Kulingana na naye, migawanyiko itakwamisha […]

JESHI LA VENEZUELA LAMTAMBUA KIONGOZI MPYA

Jeshi la Venezuela limetangaza kumuunga mkono aliyekuwa makamu wa Rais Nicolas Maduro aliyebanduliwa na Marekani, Delcy Rodriguez kuwa rais wa taifa hilo baada ya kuapishwa. Waziri wa ulinzi nchini humo Vladimir Padrino Lopez ameashiria kumuunga mkono Rodriguez ambaye rais wa Marekani Donald Trump amesema ni kiongozi mwafaka ambaye Marekani inaweza kufanya naye kazi. Kupitia hotuba […]