KLABU 16 ZASUBIRI DROO YA RAUNDI YA 16 UEFA

Lazar Samardzic alifunga mkwaju wa penalti katika dakika za mwisho na kuizamisha Borussia Dortmund ya Ujerumani waliopokezwa kichapo cha mabao 4-1 na wenyeji Atalanta wa Italia katika kipute cha kufuzu raundi ya 16 ya klabu bingwa bara Ulaya jana usiku. Dortmund waliokuwa wakiongoza mabao 2-0 kutokana na ushindi kwenye mkondo wa kwanza, walishindwa kulinda uongozi […]

SHABANA YAJIWEKA MIONGONI MWA WAWANIAJI KPL

Ushindi mwembamba wa bao 1-0 wa Shabana FC dhidi ya Mathare United uliwapandisha na kuwaweka alama sawa na AFC Leopards, na hivyo kuiweka timu hiyo katika nafasi ya kuwania taji la ligi kuu ya soka nchini, KPL. Bao la pekee la mchezo lilipachikwa wavuni na nahodha George Onyango dakika za jioni, na kuwapa vijana hao […]

ODIRA, HUNTER-BELL NA HODGKINSON KUFUFUA UHASIMU PREFONTAINE CLASSIC

Bingwa wa dunia katika mbio za mita 800, mkenya Lilian Odira ameratibiwa kufufua uhasama kati yake na Waingereza Keely Hodgkinson na Georgia Hunter-Bell, watatu hao watakapochuana katika mbio za Prefontaine Classic Julai mwaka huu. Kinyang’anyiro chao cha hivi punde ni katika mbio za ubingwa wa dunia jijini Tokyo Septemba mwaka jana, ambapo Odira aliwaonyesha kivumbi […]

MATIBABU YAENDELEA KUSAMBARATIKA NAIROBI, MARSABIT

Wakazi katika kaunti za Nairobi na Marsabit wanaendelea kutatizika kupata huduma za matibabu kwenye hospitali za umma kutokana na mgomo wa wahudumu wa afya, wanaosema hali imedorora zaidi na kuweka maisha ya wagonjwa hatarini. Kulingana na maafisa wa muungano wa wahudumu hao wakiongozwa na viongozi wa KUCO, takribani asilimia 90 ya huduma sasa hazipatikani, huku […]

FAMILIA YA JAMAA “ALIYERUSHWA’ YALILIA HAKI

Polisi wameimarisha uchunguzi katika tukio ambapo mwanamme mwenye umri wa miaka 25 alifariki baada ya kuripotiwa kurushwa nje ya basi la uchukuzi ambalo hatimaye lilimkanyaga hadi kufa kwenye barabara ya Kitengela kuelekea Namanga kaunti ya Kajiado Jumanne usiku. Familia ya Joseph Mureithi imesema kwamba jamaa yao alikuwa akirejea nyumbani kutoka kazini aliporushwa nje ya basi […]

TRILIONI 5 ZA HAZINA YA MIUNDOMBINU YAIBUA HOFU

Hofu imeibuka kuhusu kubuniwa kwa hazina ya kitaifa ya miundombinu ya thamani ya shilingi trilioni 5, watalaam wakishinikiza marekebisho ya mswada huo wa mwaka 2025-26 ili kuimarisha uwazi na uwajibikaji. Akiwa mbele ya kamati ya fedha katika bunge la kitaifa, afisi ya mdhibiti wa bajeti ya serikali imeonya kuwa hazina hiyo imebuniwa kama taasisi ya […]

“NUSU MKATE” YA ODM

Chama cha ODM kimeshikilia kuwa ni sharti kihakikishiwe asilimia 50 ya nyadhifa za serikali mbali na utekelezwaji wa ajenda 10 kabla ya kuingia kwenye ushirikiano wa kisiasa na chama cha UDA chake Rais William Ruto. Kwa mujibu wa mrengo wa kinara Oburu Oginga ukiongozwa na mwenyekiti wa chama hicho Gladys Wanga, ODM ingali serikalini na […]

UPINZANI WAKEJELI KAULI ZA RUTO

Muungano wa upinzani umejitetea dhidi ya kauli za Rais William Ruto kwamba hauna ajenda yoyote ya maendeleo, badala yake muungano huo ukimkejeli rais kwamba rekodi aliyo nayo ni ukiukaji wa haki za kibinadamu na utawala wa sheria. Viongozi wa muungano huo akiwemo Kalonzo Musyoka wa Wiper, Rigathi Gachagua wa DCP na naibu kinara wa Jubilee […]

GRIEZMANN AANZA MAZUNGUMZO NA ORLANDO CITY

Mshambuliaji Wa Ufaransa, Antoine Griezmann, anaripotiwa kufanya mazungumzo na klabu ya Orlando City SC inayoshiriki Ligi Kuu ya Soka ya Marekani. Kwa sasa Griezmann anakipiga katika klabu ya Atlético Madrid, ambako ndiye mfungaji bora wa muda wote wa klabu hiyo. Pia alifunga mabao 44 katika maisha yake ya kimataifa akiwa na timu ya taifa ya Ufaransa. […]

AYANY ATAKA NAIVAS KULIPIZA KISASI DHIDI YA LUANDA VILLA

Kocha mkuu wa Naivas FC, Elvis Ayany, amesema timu yake imejipanga kulipiza kisasi watakapokutana na Luanda Villa mwishoni mwa wiki katika mechi ya ushindani mkali ya Ligi ya Daraja la Kwanza. Ayany amesema kumbukumbu ya kichapo cha bao 1-0 walichopata katika mechi ya awali imewapa motisha ya kubadili matokeo safari hii. Hata hivyo, kocha huyo […]