SIFUNA APATA MWANGA MPYA
Katibu mkuu wa ODM na ambaye ni seneta wa Nairobi Edwin Sifuna, amepata afueni ya muda kufuatia uamuzi mpya wa jopokazi la kutatua migogoro ya vyama vya kisiasa kwamba hatua zozote za kumtimua kutoka wadhifa wa chama hicho usitishwe hadi kesi aliyowasilisha itakaposikilizwa na kuamuliwa.
Akitoa agizo hilo, kaimu mwenyekiti wa jopokazi hilo Gad Gathu, amesema licha ya ODM kuwa na uhuru wa kuendelea na mchakato wa kumwadhibu Sifuna, uamuzi wao haufai kutekelezwa hadi kesi hiyo iamuliwe.
Kesi hiyo itasikilizwa tarehe 9 mwezi ujao.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































