#Local News

UCHUNGUZI ZAIDI KUFANYIWA MWILI WA OBWAKA

Familia ya aliyekuwa mkurugenzi wa Nairobi Hospital, Daktari Job Obwaka, sasa inasubiri uchunguzi wa mwisho wa seli na tishu, mbali na kiwango cha sumu mwilini baada ya upasuaji wa maiti kuthibitisha kwamba alifariki kutokana na mshtuko wa moyo.

Wanapatholojia ambao wamebainisha kuwa mwili wake haukuwa na majeraha ya nje, wamelazimika kufanya uchunguzi huo hasa baada ya sahani mbili, kijiko, mvinyo na dawa kupatikana nyumbani kwa daktari huyo, ikiaminika kuwa alivitumia vifaa hivyo katika saa zake za mwisho.

Wakili Levi Munyeri wa mshukiwa mkuu Beatrice Wangari anayeendelea kuzuiliwa kwa amri ya mahakama, sasa maetaka mteja wake kuachiwa huru.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

UCHUNGUZI ZAIDI KUFANYIWA MWILI WA OBWAKA

SIFUNA APATA MWANGA MPYA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *